Imeandika na Sheikh Tawakkal Juma.
1. ✨ MAANA YA ZAKATUL-FITRI
Ni zaka maalumu inayotolewa baada ya kumalizika mfungo wa mwezi wa ramadhan.
- imeitwa hivyo kwa sababu inawajibika kwa kuingia siku ya idd-el-fitri.
- Piah inaitwa zaka ya viwiliwili na kufungua miili kwa sababu inawajibika kwa kila nafsi na sio katika Mali.
- Zama hii imefaradhishwa mwaka wa pili Hijiria baada ya kufaradhisha funga ya ramadhan.
2. HUKUMU YAKE
Ni wajibu kwa kila muislamu mwanaume na mwanamke, mdogo na mkubwa, aliyehuru au mtumwa anapaswa kuitoa baada ya funga ya Ramadhani kabla ya kuswali swala ya Iddil-Fitri.
- Watoto, wanawake, wazee n.k wasio na uwezo wa kulipa Zakatul-Fitri watalipiwa na mawalii wao (wasimamizi wao).
- Kwamfano katika familia baba atamtolea mkewe na watoto wake ikiwa hawawezi kujitolea, pia atawatolea wazazi wake kama nao pia hawana uwezo wa kujitolea, vilevile baba atalazimika kuwatolea Zakatul-Fitri wale wote wengine ambao ni waislamu walio chini ya uangalizi wake na hawawezi kutoa Zakatul-Fitri.
- Hata mtoto mchanga aliyezaliwa dakika chache kabla ya kuandama kwa mwezi naye pia atatolewa Zakatul-Fitri.
3. WANAOPASWA KUTOA ZAKATUL FITRI
- Zakatul Fitri inamlazimu yeyote yule mwenye kupata chakula cha kumtosha yeye na wale waliochini ya uangalizi wake kwa mchana wa siku ya Iddi na usiku wake na akawa na ziada.
- Ziada hiyo ataitoa Zakatul-Fitri kwa viwango vinavyostahiki.
4. KIWANGO CHA ZAKATUL FITRI
- (Imekuja katika mafundisho ya mtume kuwa kiwango ni Swaa’ moja) ambayo ni makadirio sawa na Kilo mbili na nusu au mchoto wa chakula wa ujazo wa viganja viwili vya mkono vya mtu wa wastani vilivyojaa mara nne.
- Kinachotolewa ni chakula Kinachotumika na watu Katika nchi hiyo
- (mfano mchele) au pia mtu anaweza kutoa kiasi cha pesa chenye thamani sawa na kiasi hicho cha chakula (kisichopungua,ni bora hata ikizidi kdg),
- mfano kilo 2 na nusu ya mchele mzuri katika eneo fulani inaweza kuwa ni Tsh 7000/= (Itategemea na eneo)
5. JINSI YA KUTOA ZAKATUL FITRI
- kwa urahisi zaidi Zakatul Fitri hukusanywa pamoja katika sehemu zenye kuaminika kama misikitini au katika taasisi za kidini na kisha kuwafikishia wahusika hivyo pia ukipata ugumu wa kumfikia mhusika wa kupewa Zakatul Fitri unaweza ukaiwasilisha sehemu hizo.
NB: Kama ukiweza ni vizuri zaidi kutoa chakula na kumfikishia mhusika moja kwa moja kama ilivyokuja kiasili katika hadith ya mtume(s.a.w), licha ya watu kuona kuwa pesa ndiyo rahisi na inapendeza zaidi hata kwa mhusika mwenyewe anayepewa Zakatul Fitri ili kupata na mahitaji mengine lakini tambua pia unaweza kutoa chakula hicho kama Zakatul Fitri kisha na pesa hiyo ya mahitaji mengine kama Sadaqa ya kawaida ambayo ni bora pia.
- Kiasi chini ya kiwango cha Zakatul Fitri na au kutoa kitu kingine tofauti na lengo la Zakatul Fitri hiyo sio Zakatul Fitri ni Sadaqa ya kawaida.
6. UMUHIMU WA ZAKATUL-FITRI
Zakatul-Fitri ni kwa ajili ya kuitakasa funga ya muislamu kutokana na maneno machafu na mambo ya upuuzi wakati alipokuwa katika swaum kwa kuwalisha maskini chakula ili nao wapate chakula kizuri siku ya Iddi na ndio maana kutolewa kwake kunakuwa kabla ya kusali sala ya Iddil-Fitri ili kuendana na maandalizi.
7 . MUDA WA KUTOA ZAKATUL-FITRI
- Muda mzuri zaidi ni wakati kuanzia Magharibi ya siku ya mwisho ya Ramadhani hadi asubuhi kabla ya Sala ya Iddil-Fitri.
- Inaweza pia kutolewa siku mbili au tatu hivi kabla (Chamsingi iwe kabla ya sala ya Iddil-Fitri).
- Kulipa Zakatul-Fitri mapema kabla ya kusali lddi au mapema zaidi ya hapo kutawawezesha maskini na mafakiri kufurahia lddi pamoja na waislamu wengine.
- Ikitokea sababu ya msingi kama vile kusahau na mtu akachelewa kutoa Zakatul-Fitri mpaka lddi ikasaliwa, basi hana budi kuitoa baada ya sala lakini jambo la kuzingatia ni kwamba amri ya kutoa Zakatul-Fitri kabla ya sala imetolewa na mtume (s.a.w) hivyo mtu akiivunja amri hii kwa makusudi au kwa uzembe ajue kuwa atakuwa amefanya makosa.
8 . WANAOSTAHILI KUPEWA ZAKATUL-FITRI
- Wanaostahiki ni maskini na wale wote wasioweza kujipatia chakula pamoja na wale walio chini ya uangalizi wa hao maskini na wasiojiweza ili nao wafurahie Iddi pamoja na waislamu wenzao wenye uwezo.
- Kama pia ilivyo katika Zakatul-Mal akipewa Zakatul-Fitri mtu asiyestahiki itakuwa ni kudhulumu haki ya wale wanaostahiki,
- hivyo mtoaji na mpokeaji wa Zakatul-Fitri hiyo wote watakuwa ni madhalimu.
- Ili kuhakikisha kuwa katika jamii au katika mtaa wa waislamu kila anayestahiki kupewa Zakatul-Fitri anapata na kuzuia uwezekano wa mtu mmoja kulundikiwa Zakatul-Fitri kiasi kikubwa sana na mwingine kukosa au kupata kiasi kidogo sana kisichotosheleza mahitaji yake ya siku ya Iddi,
- basi ni vyema waislamu wa sehemu hiyo waikusanye Zakatul-Fitri kwa pamoja na kisha waigawanye kwa wote wanaostahiki katika mtaa au sehemu hiyo wakizingatia mahitajio yao kulingana nao majukumu ya kifamilia waliyonayo.
- Piah inajuzu kumpa mtu mmoja zaidi ya pishi moja
- Muislamu inampasa achukue juhudi ya kuwatafuta wanaostahiki kupewa zaka hii.
NB:Watu unaowajibika kuwatolea Zakatul-Fitri haihesabiki kuwa unawapa Zakatul Fitri, mfano kuwapa wazazi wako sio Zakatul-Fitri kwani wao ni wajibu wako kuwahudumia.
The primary purpose of this blog is to share latest information, opinions, exchange knowledge and expertise on the field of Islamic Finance from different perspectives. The secondary purpose is to share opinions and key development of Islamic Banking and Islamic insurance in Tanzania.
Tuesday, March 25, 2025
SUKUK NI WIZI NA UTAPELI?
Nimeona katika mitandao ya kijamii maneno ambayo hayapaswi kukaliwa kimya hususani na wadau wa sekta ya fedha ya Kiislam. Maneno hayo anuani yake ni "SUKUK NI WIZI NA UTAPELI, BENKI KUU TOENI TAHADHARI" ukiwa "unaonekana" kuingiza Sukuk katika kinyang'anyiro cha mashindano ya Kisiasa visiwani Zanzibar lakini pia huenda waandaaji wake wana malengo ya kutia hofu wananchi dhidi ya hatua kubwa iliyofikiwa nchini ya kuwa na Sukuk iliyotolewa na SMZ. Tunajiuliza dhamira gani waliyonayo wale walioandaa ujumbe huo? Kwa nini katika mikopo yote ya serikali ya Zanzibar hatujasikia kunasibishwa na Wizi na Utapeli isipokuwa Sukuk?
Waingereza wanamsemo wao "If you want to kill a dog, give it a bad name (ukitaka kumuua mbwa, mpe jina baya)." Kuinasibisha sukuk na wizi na utapeli ni katika mkakati mbaya sana na haunabudi kukemewa vikali na wadau wote wa maendeleo jumuishi katika nchi yetu. Nakemea kitendo hicho ambacho sio cha kistaarabu wala uungwana, huku nikiwa na matumaini kuwa vyombo vya usalama vitakuwa mbioni kuwatafuta watu waliopo nyuma ya ujumbe huo na kuwachukulia hatua stahiki.
Sitoingia katika ujumbe wa kisiasa uliovikwa tu ndani ya ujumbe huo, bali ninachokiona ni mashambulizi dhidi ya Sukuk kama njia mbadala na jumuishi kwa maendeleo ya nchi yetu. Hivyo, niseme kuwa kwa mujibu wa mpango wa maendeleo wa miaka mitano (FYDP), Sukuk inatambulika na mamlaka za nchi kama njia mbadala wa kuwezesha maendeleo ya nchi yetu. Zanzibar Sukuk ni hatua kubwa katika kutekeleza mpango huo na inatambulika na Benki Kuu na Mamlaka ya Masoko ya Fedha na Mitaji nchini. Hivi karibuni, tumeona Gavana wa Benki Kuu akiwa na Waziri wa Fedha wa Zanzibar akipendekeza wananchi wawekeze katika Sukuk hiyo. Hivyo, ni hujuma mbaya sana kutumia upotoshaji kwa lengo si tu la kupata kiki ya kisiasa bali kuichafua Sukuk kama njia jumuishi na inayotambulika nchini. Wale walionyuma ya ujumbe huo, waache mwenendo huo ambao unaathari mbaya sana katika kujenga jamii ya watu wastaarabu, maendeleo endelevu na utoaji wa huduma jumuishi za kifedha nchini.
Kwa upande mwingine, ujumbe huo umedhihirisha na kutukumbusha kiasi gani Siasa inavyoweza kuathiri huduma za kifedha za Kiislam ktk nchi zetu. Binafsi, imenikumbusha kitabu cha Prof Rodney Wilson, The Politics of Islamic Finance akionesha namna gani Siasa za nchi zinaweza kuathiri vizuri au vibaya maendeleo ya Islamic Finance. Kwa muktadha huo, hatupaswi kukaa kimya pale tunapoona watu wachahe wanataka "kutumia siasa chafu" katika jambo muhimu kama hili lenye kujumuisha na kuwapa watu fursa kushiriki katika maendeleo ya nchi yao na kukuza vipato vyao kwa njia Halali bila Riba!
Kwa kuhitimisha, mara zote tumeona athari chanya ya utashi mzuri wa kisiasa kupitia ilani za vyama vya Siasa na utekelezaji wake katika kuwezesha huduma za kifedha za Kiislam nchini kustawi na kunufaisha wananchi. Wote walionyuma ya utashi huo mzuri, tunawapongeza na kuwataka wasikatishwe tamaa kwa hali yoyote iwayo. Hii ni mara ya kwanza natumai itakuwa ya mwisho, kuona watu kupitia "mlango wa kisiasa", wakihusisha Sukuk na wizi au utapeli. Waislam na hususani wataalamu wa masuala ya kifedha ya Kiislam, hatuwezi kukaa kimya na kukubali upotoshaji huo kwa kupitia mlango wa Kisiasa ambao unahujumu au kurejesha nyuma juhudi za miongo kadhaa zenye dhamira ya kutoa fursa kwa Waislam na wananchi wengine kushirikiana na Mamlaka za nchi yao katika upatikanaji wa huduma jumuishi za kifedha nchini.
Waingereza wanamsemo wao "If you want to kill a dog, give it a bad name (ukitaka kumuua mbwa, mpe jina baya)." Kuinasibisha sukuk na wizi na utapeli ni katika mkakati mbaya sana na haunabudi kukemewa vikali na wadau wote wa maendeleo jumuishi katika nchi yetu. Nakemea kitendo hicho ambacho sio cha kistaarabu wala uungwana, huku nikiwa na matumaini kuwa vyombo vya usalama vitakuwa mbioni kuwatafuta watu waliopo nyuma ya ujumbe huo na kuwachukulia hatua stahiki.
Sitoingia katika ujumbe wa kisiasa uliovikwa tu ndani ya ujumbe huo, bali ninachokiona ni mashambulizi dhidi ya Sukuk kama njia mbadala na jumuishi kwa maendeleo ya nchi yetu. Hivyo, niseme kuwa kwa mujibu wa mpango wa maendeleo wa miaka mitano (FYDP), Sukuk inatambulika na mamlaka za nchi kama njia mbadala wa kuwezesha maendeleo ya nchi yetu. Zanzibar Sukuk ni hatua kubwa katika kutekeleza mpango huo na inatambulika na Benki Kuu na Mamlaka ya Masoko ya Fedha na Mitaji nchini. Hivi karibuni, tumeona Gavana wa Benki Kuu akiwa na Waziri wa Fedha wa Zanzibar akipendekeza wananchi wawekeze katika Sukuk hiyo. Hivyo, ni hujuma mbaya sana kutumia upotoshaji kwa lengo si tu la kupata kiki ya kisiasa bali kuichafua Sukuk kama njia jumuishi na inayotambulika nchini. Wale walionyuma ya ujumbe huo, waache mwenendo huo ambao unaathari mbaya sana katika kujenga jamii ya watu wastaarabu, maendeleo endelevu na utoaji wa huduma jumuishi za kifedha nchini.
Kwa upande mwingine, ujumbe huo umedhihirisha na kutukumbusha kiasi gani Siasa inavyoweza kuathiri huduma za kifedha za Kiislam ktk nchi zetu. Binafsi, imenikumbusha kitabu cha Prof Rodney Wilson, The Politics of Islamic Finance akionesha namna gani Siasa za nchi zinaweza kuathiri vizuri au vibaya maendeleo ya Islamic Finance. Kwa muktadha huo, hatupaswi kukaa kimya pale tunapoona watu wachahe wanataka "kutumia siasa chafu" katika jambo muhimu kama hili lenye kujumuisha na kuwapa watu fursa kushiriki katika maendeleo ya nchi yao na kukuza vipato vyao kwa njia Halali bila Riba!
Kwa kuhitimisha, mara zote tumeona athari chanya ya utashi mzuri wa kisiasa kupitia ilani za vyama vya Siasa na utekelezaji wake katika kuwezesha huduma za kifedha za Kiislam nchini kustawi na kunufaisha wananchi. Wote walionyuma ya utashi huo mzuri, tunawapongeza na kuwataka wasikatishwe tamaa kwa hali yoyote iwayo. Hii ni mara ya kwanza natumai itakuwa ya mwisho, kuona watu kupitia "mlango wa kisiasa", wakihusisha Sukuk na wizi au utapeli. Waislam na hususani wataalamu wa masuala ya kifedha ya Kiislam, hatuwezi kukaa kimya na kukubali upotoshaji huo kwa kupitia mlango wa Kisiasa ambao unahujumu au kurejesha nyuma juhudi za miongo kadhaa zenye dhamira ya kutoa fursa kwa Waislam na wananchi wengine kushirikiana na Mamlaka za nchi yao katika upatikanaji wa huduma jumuishi za kifedha nchini.
Subscribe to:
Posts (Atom)