Pages

Saturday, December 5, 2020

SHARI'AH GOVERNANCE IN UGANDA ISLAMIC BANKING REGULATION OF 2018

"Shari'a-compliance is the backbone of Islamic banking and finance. It not only gives legitimacy to the practices of Islamic banking and finance, but also boosts the confidence of the shareholders and the public that all the practices and activities are in compliance with Shari’a at all times. The existence of non-Shari’a-compliant element would not just affect the confidence of the public but might also expose Islamic financial institutions (IFIs) to fiduciary and reputational risks. Compliance with the Shari’a principles will be achieved through having a proper Shari’a governance framework in placed." Above quotation explains the reason of having robust Shari'ah governance as a regulatory requirement besides being the best practice. SHARIA SUPERVISORY / ADVISORY BOARD. In East African region, IFIs constitute Shari'ah governance to conform with best practices with exception of Uganda which has issued Islamic banking regulations in 2018 therein Shari'ah governance is recognised as crucial component of Islamic banking. Clause 12 of the regulation states "Every financial institution which conducts Islamic financial business shall appoint and maintain a Shari’ah Advisory Board in accordance with section 115B of the Act." The act stipulates that SAB shall be appointed by the board of directors, answerable to them, they must be between 3 to 5 members, their qualifications, SAB main functions and must be vetted by the Central bank. Besides institutional SAB,the Central Bank shall establish central Shariah advisory board in order to approve products and advise CBU on matters of regulation and supervision. SHARIAH AUDIT. The regulation require establishment of Shari'ah audit function, it states "A financial institution carrying on Islamic financial business or a financial institution operating an Islamic window shall conduct a Shari’ah audit on a periodical basis." Besides, the regulation articulates the scope of the Shariah audit for IFIs. EVALUATION OF THE SHARI'AH GOVERNANCE Sharia advisory board and Shari'ah audit are the only two internal organs identified by the regulation for Shari'ah governance. Where as this minimalist approach is commendable, financial institutuins offering or planning to offer Islamic financial services must consider other critical functions in accordance with industry practices. This includes establishment of Shari'ah compliance unit that is responsible with day to day Shari'ah oversight, advisory and training for the entire bank staff. SUGGESTIONS TO IMPROVE THE REGULATIONS. It is also important to mention that the regulations have some weaknesses which need to be addressed. These are; 1. Clause 12 mention that appointment of SAB should be in accordance with section 115B of the Financial Institution Act. I have failed to identify this section in the Act as there is 115 but no 115B, thus making it difficult to understand fully section requirement with regards to SAB appointment. This section needs to be clarified. 2. SAB members are subjected to approval by Central Bank. In my view, Central Bank should limit itself to articulating qualifications of members of SAB and require banks to ensure those appointed meets those qualifications. This will reduce gov't bureaucracy or feeling of interference on this organ. Alternatively, vetting of members of SAB should be done by Central Sharia Advisory Council rather than Central Bank. 3. The regulation doesnot give any powers to the SAB on matters under its mandate. What if the management doesnot fulfill the advise or guidelines issued by SAB? 4. The functions of SAB have been extremely limited to "... advise, approve and review the Islamic financial business of a financial institution in order to ensure that the Islamic financial business of the financial institution complies with the Shari’ah." The regulation should borrow from AAOIFI on functions of Shari'ah Supervisory Board. 5. With regards to reporting of Shari'ah audit functions, it is recommended that they shouls also report to Board of Director's Audit Commettee since it has the power to enforce corrective measures. 6. Removal of member of SAB should not be left to BOD without Central SAC oversight. Hence it is recommended that such removal should be subjected to no objection from the Central SAC to ensure SAB independence and security of tenure. 7. The regulation is totally silent on who is responsible to ensure Shari'ah compliance in the banks. Is it the BOD? Is it the Management? is it the SAB? It is important to state that the management is fully responsible to ensure Shari'ah compliance. 8. Reporting on Shari'ah compliance should not be done by BOD as stated in clause 17. "The regulation requires BOD in respect of the financial statements of the financial institution, report at least once a year, on the Shari’ah compliance of the financial institution." This is not BOD mandate. It is only SAB that shoud have such mandate in order to provide assurance, promote transparency and gain public confidence. According to AAOIFI and the best practice, SAB is the one that must provide such a report annually. On Central Shari'ah Advisory Council, it is recommended that: 1. Clause 18 should have (c) to review on proposed members of institutional SAB members. Though as earlier stated it is good for Central Bank not to get involved with appointment. (d) Receive and review reports of outstanding Shari'ah audit issues not resolved within specified period of time. 2. Clause 19, it is a grave mistake to give chairmanship to the Governor of the Central SAC. Given what it is supposed to do under clause 18, it is extremely unprofessional to have Central Bank officials to constitute the majority in council. This is a Council of Shari'ah Scholars and must remain so. Such diffusion with Central bank official must be corrected. Central bank officials should only be invited guests but with no specific role neither voting power to the decisions of the Council. As it is now, out of 5 members only two are Shari'ah scholars. Is it central Shariah advisory council or it is another committee of the Governor? 3. It is not clear what relationship does the Central SAC have with the Central Bank Board of Director that is entrusted to appoint them? To whom does the council reports to? It is also not clear if non-Ugandan can serve in the SAB and in the Central SAC given that the qualifications required may be short in supply in Uganda. In conclusion, as earlier said, government of Uganda has taken examplary step in regulating Islamic banking in the region and thus sets an example for other neighbouring countries to follow. Therefore, it must ensure it gets it right and hence above suggestions aims to improve the regulation so that we operate within international best practices without ignoring our context. Note: I am oepn to support organs interested on setting up regulations for Shari'ah governance of Islamic Financial Institutions as well as help Islamic Financial Institutions to have robust Shariah governance framework. Those interested can contact me through: kmgeituff@gmail.com

Sunday, November 15, 2020

MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI: FURSA, CHANGAMOTO NA UFUMBUZI WAKE

Moja katika mambo yanayopaswa kupongezwa kwa serikali na wabunge ni kuwepo kwa Sheria ya Fedha za Serikali za mitaa (Chapter 290- The Local Government Finance Act 2019) na hususani kifungu 37 A ambacho kinasema kwamba (tafsiri ni yangu): 1. Mamlaka za serikali za ndani (district authority and urban authority) watateenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya kuwezesha vikundi vilivyosajiliwa vya kina mama, vijana na watu wenye ulemavu. 2. Fedha zote zitakazotengwa kwa mujibu wa kifungu (1) zitatumika kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vilivyosajiliwa vya wanawake, vijana na wau wenye ulemavu kwa mgao wa asilimia 40 kwa wanawake, asilimia 40 kwa vijana na asilimia 20 kwa wenye ulemavu. 3. Mikopo itakayotolewa kwa mujibu wa kifungu hiki haitakiwi kutozwa RIBA 4. Waziri, kwa kupitia kanuni anaweza kuweka utaratibu wa usimamizi na ugawaji wa mikopo hiyo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. FURSA. Kwa kuzingatia amri ya Sheria hii, fursa ya kupata mikopo ambayo haina riba kwa wananchi inapaswa kutumika ipasavyo kwa mujibu wa taratibu ambazo wilaya husika kwa kupitia mamlaka aliyopewa Waziri husika itaziweka. Ni wajibu wa serikali za wilaya kuweka wazi uwepo wa fedha hizi na taratibu zake zote katika tovuti, na machapisho ya wilaya husika ili wananchi waweze kujuwa kiwango cha fedha kilichotengwa kwa mwaka husika, mchakato wa maombi, muda wa kujibiwa maombi, shughuli za uzalishaji au biashara zinazopewa kipaumbele na kadhalika. Kadhalika ni wajibu wa madiwani, kuhakikisha wilaya husika inaweka wazi taarifa zote za mikopo hii kwa wananchi na yeye kuzifikisha taarifa hizo kwa makatibu watendaji wa kata, wenyeviti wa serikali za mitaa na kwa mabalozi wa nyumba kumi. Kadhalika ni wajibu wa watumishi hawa bila kujali mrengo wa kisiasa wa wananchi anao wawakilisha kuzifikisha taarifa hizo ili wananchi wote wanufaike kwa kukuza uzalishaji na kukuza biashara katika maeneo husika. Kama wananchi, ni wajibu wetu kujiunga katika vikundi kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na halmashauri husika kwa jili ya kuweza kupata mikopo hii na kujikomboa kiuchumi. CHANGAMOTO. Katika mkutano wa mwisho wa mwezi wa Oktoba, taasisi ya Policy Forum kwa kushirikiana na UNA Tanzania waliaandaa mjadala kuhusu mikopo hii ya asilimia kumi. Ndugu Maeda aliwasilisha mada nzuri juu uwepo wa fursa hii kwa wananchi na changamoto kadhaa zikiwemo 1. Kutotekelezwa kwa amri ya sheria hii kwa baadhi ya wilaya nchini. 2. Kukosekana kwa taarifa kwa wananchi wa wilaya husika juu ya uwepo wa mikopo hii kwa vikundi. Tafiti yangu ndogo kwa njia ya mtandao kwa wilaya zote za Dar es Salaam, tovuti zao hazina taarifa hii katika huduma zao kwa wananchi. Wilaya ya Kigamboni tu kwa kupitia jarida lao la mwaka huu lililopo katika tovuti ya Tamisemi inaonesha kuwa kuanzia mwaka 16/17 mpaka 19/20 jumla ya Bil 1.4 zimetumika kwa ajili ya mikopo hiyo. Hatahivyo hamna taarifa zozote kuhusu kanuni na taratibu za utoaji na upatikanaji wa mikopo hiyo ya vikundi katika jarida hilo na mengineyo katika tovuti zao. 3. Uhaba wa rasilimali watu katika halmashauri kwa ajili ya kusimamia kanuni, taratibu na urejeshaji wa mikopo hiyo. Maafisa maendeleo ya jamii ambao wamepewa jukumu hili pamoja na majukumu mengine wanahemewa na uzito wa kazi na hivyo kupelekea usimamizi legevu wa mikopo hiyo katika utoaji wake na ufuatiliaji wa urejeshwaji wake. Suala la utoaji mikopo na usimamizi wake (Credit Management Skills) ni la kitaalamu na lenye kuhitaji weledi mkubwa katika kulifanikisha. Ukosefu wa muda na mafunzo hayo ni kikwazo kikubwa sana. 4. Vikundi hewa vinavyohusishwa na wanasiasa waliopo madarakani katika wilaya husika ni tatizo kubwa. Hii inapelekea fedha zinazotolewa kutokurudishwa na hamna taarifa rasmi ya urejeshwaji wa mikopo hiyo. Halmashauri nyingi zinaeleza kiwango cha utoaji wa mikopo husika na hawaelezi makusanyo ya madeni hayo. Kwa nini? 5. Utowaji wa mikopo kwa mrego wa kisiasa ni tatizo kubwa. Baadhi ya wanasiasa, kama wabunge na madiwani, wanaweza kugeuza kuwa mtaji wa kisiasa katika utoaji wa taarifa za uwepo wa mikopo hii, kutowa ushawishi wa vikundi vya kupewa na visivyofaa kupewa, kujitafutia umaarufu wa kisiasa kwa kupitia mikopo hiyo na hata kushawishi kuundwa vikundi hewa ili walengwa wao wanufaike. 6. Muda mfupi wa kuanza marejesho ya mikopo husika. Kwa kukosekana weledi katika fani ya mikopo, mikopo hutolewa bila kuzingatia mzunguko wa biashara husika. 7. Muda mrefu wa kujibiwa maombi ya mikopo. 8. Uwezo mdogo wa kiungozi wa kuendesha miradi ya vikundi husika. Vikundi husika kwa kukosa maarifa ya somo la biashara na ujasiriamali na uongozi, wanashindwa kuendesha biashara na vikundi vyao kufikia malengo ya miradi ya vikundi. Watendaji wa vikundi hawana ujuzi wa usimamizi wa fedha, undeshaji wa miradi ya kiuchumi na masuala ya uongozi. 9. Urasimu katika mchakato wa kupata mikopo. Hili ni changamoto kongwe katika shughuli za halmashauri ambao unatokana na kuwepo kwa masharti ambayo hayanatija zaidi ya upotevu wa muda. Kwa mfano, maombi ya mikopo yatakiwa iambatane na barua ya utambulisho wa mtendaji wa kijiji au mtaa na mtendaji wa kata. Mara nyingi ofisi za watendaji hao zipo maeneo tofauti na kila mtendaji kabla ya kutoa utambulisho huo anachukuwa siku kadhaa na hata kupelekeya hisia za kutaka rushwa ili kuandika barua hiyo. 10. Upo uwezekanao wa halmashauri kutoza riba katika mikopo hii kinyume na sheria iliyotajwa hapo juu. SULUHISHO. 1.Taarifa kwa wananchi. Halmashauri zote zinapaswa kuweka taarifa za uwepo wa mikopo hii katika tovuti zao, mabango ya halmashauri na machapisho ya halmashauri. Taarifa za kina zenye kueleza kanuni na taratibu zote za upatikanaji na utoaji wa mikopo hiyo kwa njia ya uwazi na uwajibikaji. Tovuti za Halamshauri nyingi nchini hazina taarifa zozote katika "Huduma Zetu" kuhusu mikopo hii. Kipekee niitaje Halmashauri ya Jii la Tanga ambao katika huduma zetu wameweka "Uwezeshaji wananchi." Hatahivyo, taarifa zao zinahitaji kuboreshwa zaidi ili kuwe na uwazi. 2. Mrengo wa Kisiasa. Wizara na Wakuu wa Mikoa yote husika wanapaswa kuhakikisha ya kuwa Halmashauri hazitowi huduma hii kwa mrengo wa kisiasa. Kama ambavyo benki hutakiwa kuanisha mikopo kwa wanasaisa, kadhalika mikopo inayotolewa kwa vikundi vinavyohusiana na wanasiasa yapaswa taarifa hizo kuwekwa wazi na umakini katika kuongeza uchambuzi wa tathmini ya miradi husika ili kuepusha tatizo la vikundi hewa au vikundi vya kisiasa ambayo mikopo hiyo huwa ni kama zawadi badala ya kufanyia shughuli za kiuchumi. 3. Elimu ya Biashara na Uongozi. Kitaifa elimu ya biashara na ujasiriamali ni muhimu sana haswa ukizingatia kuwa sekta binafsi na ujasiriamali ni injini ya uchumi wa kisasa kama alivyosema Mh. Rais katika ufunguzi wa bunge la 12. Kadhalika elimu ya uongozi wa vikundi ni nguzo muhimu katika kufanikiwa kwa kikundi cha kiuchumi. Mkakati wa muda mrefu unahitaji kuwepo somo la biashara lianze kufunzwa katika elimu ya msingi na iwe lazima mpaka kidato cha nne. Somola General Studies katika A' level lazima liwe na maudhui ya Ujasiriamali wenye mafanikio na uongozi wa vikundi vya kiuchumi. Kadhalika, mkakati wa muda mfupi unahitaji kuzilazimisha Halmashauri kwa kushirikiana na taasisi binafsi na za umma za kutowa mafunzo ya ujasiriamali na uongozi kwa vikundi vya kiuchumi vinavyosajiliwa katika halmashauri na wahusika wafaulu vizuri kabla ya kupewa mikopo hiyo. 4. Usimamizi wenye weledi. Maafisa maendeleo ya jamii wapate wasaidizi au waajiriwe maafisa wa mikopo ya vikundi vya kiuchumi kwa ajili ya kushughulikia kata maalumu. Maofisa hao wawe wamesomea masuala ya usimamizi makini wa mikopo ya vikundi, wawe na mafunzo ya mara kwa mara, wapewe malengo ya kila mwaka katika kutoa mikopo iliyo safi, wafuatilie mikopo, wale watakaobainika kushindwa kusimamia urejeshwaji wa mikopo hiyo waachishwe kazi na waajiriwe watendaji wengine watakaomudu majukumu yao ipasavyo. Pendekezo hili linatoa fursa kwa vijana wetu waliosoma fani za kibenki, fedha, n.k kupata ajira na fedha hizi zilizotengwa katika kutowa mikopo hii zinaweza kutumika kwa kiwango cha asilimia 30 kulipa mishahara yao na asilimia 70 kutoka katika mapato mengine ya halmashauri. 5. Kushirikiana na sekta binafsi. Ili kuepuka mikopo hewa na watu wasiokuwa waaminifu, Halmashauri na ofisi za mkoa ziwe na mashirikiano na mashirika binafsi ya kukagua taarifa za vikundi, kufuatilia mikopo sugu na kuwapeleka wahusika mahakamani. Kadhalika, kuwa na mashirikiano na vyuo vya mafunzo. 6. Tehama. Ili kuwe na ufanisi wa usimamizi mzuri, ni vyema halmashauri kutumia tehama ya usimamizi wa mikopo (credit management software) ili taarifa zote za mikopo yote iwepo katika mtandao ili kuhakikisha ya kwamba taarifa za vikundi hazipotei na utunzaji wa kumbukumbu zote unaimarishwa. 7. Adhabu na Pongezi. Wizara yapaswa kuziadhibu Halmashauri zote ambazo zitashidwa kutoa mikopo hii kwa asilimia 80% ya fedha zilizokusanywa katika mwaka husika na zile zote ambazo mikopo mibaya ni zaidi ya asilimia 10% ya fedha zilizotolewa. Wizara iwe inafanya uchunguzi wake kabla ya kutoa adhabu hizo ili kubaini changamoto ambazo zipo nje ya uwezo wa Halmashauri na kubuni namna bora ya kuzisaidia au kushirikisha sekta binafsi katika utatuzi wake. Kadhalika, wahusika wa utoaji mikopo inayotolewa nje ya taratibu na kanuni yapaswa kuadhibiwa. Na halmashauri zinazotekeleza vyema usimamizi wa mikopo hii kupongezwa na kutambuliwa. 8. Kuondoa Urasimu na kuharakisha uoaji wa huduma. Utarataribu wa wajumbe wa vikundi upunguzwe kutoka watu 10 mpaka 5, muda wa kutoa mikopo ndani ya miezi mitatu upunguzi mpaka ndani ya mwezi mmoja, na mianya ya rushwa izibwe kwa kuwa na dirisha katika halmashauri la malalamiko yote yanayohusiana na mikopo ya vikundi. Malalamiko hayo, yashughulikiwe kwa haraka na kwa uadilifu pale inapothibiti ukiukwaji wa taratibu na kanuni zilizowekwa. Hitimisho. Kwa dhati nirejee kupongeza kwa kuwepo kwa sheria hiina kwa kuwaletea wananchi fursa muhimu ya kujiwezesha kiuchumi kwa kupitia halmashauri zao nchi nzima. Kwa miaka mingi wananchi wanalalamikia riba kubwa katika taasisi za fedha na kwa hatua hii ni wazi kuwa serikali imeleta ufumbuzi mzuri ambao yatupasa kuuimarisha na kuudumisha kwa vizazi vya leo na kesho. Nitoe wito kwa taasisi nyingine kama za SIDO na mifuko mbalimbali ya uwezeshaji, kuachana na fikra mgando za mikopo ya riba bali wajikite katika kufanya biashara kwa njia ya kugawana faida au hasara (profit and loss sharing) ambayo ni yenye uadilifu, haki na jumuishi kwa wananchi wote. Mwisho, niwakumbushe maneno ya Mh.Raisi JPM akifungua bunge la 12 aliposema "Penye kukosoa kosoeni kwa hoja na kutoa mapendekezo ya namna ya kushughulikia. Tunahitaji constructive criticism na sio kukosoa kwa lengo la kukosoa tu." Haya ni maneno mazito ambayo yanatukumbusha wajibu wa kila mmoja wetu kama wananchi na sio kwa wabunge pekee. Hii ni kazi ya kila raia mwema kwa nchi yake kuhakikisha mikopo ya 10% inafanya kazi iliyokusudiwa ya kuleta mapinduzi ya kiuchumi kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Wednesday, September 23, 2020

ILANI ZA VYAMA KWA JICHO LA UCHUMI WA KIISLAMU- SEHEMU YA PILI

Wiki iliyopita tulifafanuwa ilani ya chama cha mapinduzi kuhusu sekta ya fedha kwa jicho la uchumi wa Kiislamu. Katika makala haya tutatazama vyama mbadala au maarufu kama vyama vya upinzani. Kwa kuwa vyama hivi vipo vingi tutatazama vile ambavyo ni vyenye wabunge katika bunge la Jamhuri ya Muungano. Tutaanza na CHADEMA. VIPAUMBELE VYA CHADEMA. Ilani ya Chadema ukurasa wa tani imaainisha vipaumbele 20. Kati ya vipaumbele ishirini, zaidi ya vipaumbele kumi vinahusu masuala ya uchumi na biashara. Baadhi ya vipaumbele hivyo ni:Kwa kushirikiana na sekta binafsi Kujenga uchumi imara wa kidigitali na shirikishi, Kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje, Kuwajengea uwezo wanawake kusimamia na kumiliki uchumi, Kuwezesha Wananchi kumiliki ardhi kwa matumizi endelevu,Kuboresha sekta ya madini na kuwezesha wachimbaji wadogo wanashiriki na kumiliki uchumi wa madini. SEKTA YA FEDHA. Kama ilivyo kwa ilani ya CCM, ilani ya chadema inatambuwa umhimu wa sekta ya fedha. Ilani inasema katika ukurasa 23 "Sekta ya fedha iliyo imara katika nchi, ni nguzo imara katika kuhakikisha uchumi wa nchi unashamiri na unakuwa endelevu. Sekta binafsi iliyo imara inajengwa na sekta fedha, hivyo basi sekta hii ni muhimu sana katika kujenga uchumi." Ilani hiyo pia imebainisha kuwa pamoja na kuwa na mabenki mengi nchini lakini changamoto kubwa ni " kwa wananchi kupata mikopo kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza biashara." Vile vile ilani imebainisha kuwa "kumekuwa na vikwazo vingi na vikubwa kwa wajasiriamali wapya kwenye soko katika kupata mitaji. Jambo hili kwa upande mmoja ndio kisababishi kikubwa cha uwepo wa kundi kubwa la vijana wasiokuwa na ajira hapa nchini." Kadhalika ilani inabainisha kuwa "Changamoto hizo zinatokana na sera za fedha zinazotolewa na benki kuu kwa taasisi za fedha na hivyo kuwa ni kikwazo kikuu kwa mabenki kuweza kukopesha wajasiriamali wapya JE NINI CHADEMA ITAFANYA? Ilani imeahidi mambo kadhaa ambayo ni mazuri lakini yapo ambayo kwa jicho la uchumi wa Kiislamu hazifai kabisa hususani kwa jamii ya Waislam nchini. Hatuwa nzuri zilizobainishwa na ilani ni kama vile; Mosi, Serikali ya Chadema kwa kushirikiana na sekta binafsi itatunga sera za kuwawezesha wananchi kushiriki na kunufaika na biashara ya masoko ya fedha inayotumia mitandao(ushiriki wa masoko ya hisa ya kimataifa kwa kutumia mitandao). Pili, Serikali ya Chadema itahakikisha kwamba kipaumbele cha kwanza kwa taasisi za fedha kiwe ni kuhudumia wananchi kabla ya kuhudumia Serikali. Tatu, Chadema itahakikisha kuwa kunakuwa na urahisi wa upatikanaji wa huduma za benki na fedha kwa ajili ya kusaidia wananchi kukuza biashara zao na kadhalika. Hata hivyo, hatuwa ambayo haifai ni ile isemayo "Kutenga kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya mikopo yenye masharti na riba nafuu, itakayoshindaniwa na vijana kwa ajili ya kupata mitaji na kuweza kujiajiri na kutoa ajira." Kutenga kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya mikopo yenye masharti nafuu na kupatikana kwa njia ya ushindani, hii ni sawa lakini mikopo yenye riba nafuu, hili la kutoza riba ni dosari inayoashiria kuwa watunga ilani hawajatambuwa tatizo la riba na ukubwa wake kiuchumi, hawajatambuwa uwepo wa njia mbadala isiyotoza riba na kubwa zaidi hawajatambuwa kuwa kijamii ipo sehemu kubwa ya wananchi ambao HAWAIKUBALI mikopo yenye riba nafuu au ghali. Ni dhambi kubwa kukopa kwa riba! MAPENDEKEZO. Pamoja na ilani kuonesha kuguswa na tatizo la umasikini na ukosefu wa mitaji ya kutosha kwa wananchi, ni wazi kuwa iwapo biashara ya kibenki na bidhaa zile zile za kibenki zitawachwa kama zilivyo sasa za kutoa mikopo ya riba (compunded interest) hatutatatuwa changamoto zilizopo katika sekta ya fedha kwa ukamilifu wake kwa sababu sehemu ya jamii haitokubali kushiriki katika mikopo ya aina hiyo. Inapendekezwa sekta ya fedha katika shughuli zake za uwekezaji kufungamanishwa na sekta ya vitu halisi (real economy) kwa kuwa na sera inayoitaka sekta ya fedha kama vile benki na taasisi za mikopo midogo (microfinance institution), masoko ya mitaji kugawana faida na hasara (risk sharing) na wateja wake kutokana na uwekezaji ambao benki au taasisi husika inafanya na sio kama ilivyo sasa ambapo benki inamwachia mkopeshaji kubeba hatari zote za biashara husika (risk transfer). Vile vile, kuzitaka benki zifanye biashara halisi ya vitu au utoaji wa huduma kwa kwa njia ya mauziano ya vitu kwa faida au kukodisha rasilimali kwa faida na sio biashara ya fedha kwa fedha ambayo ni jambo lisilokubaliwa katika uchumi wa Kiislam. Jambo la mwisho, inapendekezwa kuwa hatuwa mbalimbali zilizoanishwa kuwa na muda maalum wa utekelezaji na sio ahadi zisizokuwa na ukomo wa muda wa utekelezaji. Ahadi za namna hiyo zinafunguwa mlango wa kutowajibika ipasavyo na Serikali kuona inayo muda mwingi. Kwa mfano, ilani inaahidi kuwa "Serikali ya Chadema itaanzisha maeneo maalum (Kisiwa cha Mafia na Pemba) ya mitaji isiyotozwa kodi (tax heaven) ili kupanua wigo wa kupata mitaji kwa ajili ya miradi mikubwa na wajasiriamali wadogo." Je ndani ya muda gani hili litatekelezwa? Muda wa utekelezaji unapaswa kubainishwa kwa uwazi kwa wananchi.

Monday, September 14, 2020

ILANI ZA VYAMA KWA JICHO LA UCHUMI WA KIISLAMU- SEHEMU YA KWANZA

Wiki iliyomalizika vyama mbalimbali vimezinduwa kampeni na ilani zao. Ilani ni maandiko muhimu. Katika siasa, ilani ndio mkataba unaotumiwa na chama cha siasa na kujifunga na wananchi katika kipindi fulani. Vyama vilivyozinduwa ilani hizo ni pamoja na CCM, CHADEMA, ACT WAZALENDO na vinginevyo japokuwa havitajwi sana na vyombo vya habari nchini. Kama wananchi na waislamu tunatakiwa tusome ilani hizo na kuzichambuwa iwapo zinakidhi mahitajio yetu na zinatupeleka katika kujenga nchi ambayo wananchi wake wanafursa sawa za kiuchumi, kijamii na kadhalika. Kubwa zaidi ni kutazama iwapo vyama husika vinalenga kutumikiya wananchi bila ya kumuudhi Muumba wetu kwa yale ambayo inakusudiya kuyafanya au kutoyafanya katika kipindi cha miaka mitano ijayo (2020-2025). Wanasiasa na watu kwa kawaida wanaona kuwa ilani nzuri ni ile inayokelezwa na ilani mbaya ni ile ambayo haikutekelezwa. Hatahivyo, katika mizani ya Uchumi wa Kiislamu, ilani nzuri ni ile ambayo vipaumbele vyake vya kiuchumi na sera zake za fedha zinazingatia uadilifu na kutovunja amri za Muumba wetu. ILANI YA CCM NA VIPAUMBELE VYAKE. Kwa kuanzia na ilani ya CCM ambayo ndio chama kinachoongoza serikali kwa sasa kuna maandiko mawili yanayoelezeya ilani yao. Andiko la kwanza ni ilani yenyewe yenye kurasa 308 na la pili ni muhtasari wa ilani wenye kurasa 19. Katika ilani kuna mengi ambayo yanastahili kuchambuliwa lakini makala haya yanalenga katika kutazama ilani hii inasemaje kuhusu Uchumi wa fedha au sekta ya fedha (Financial Economy or Sector) kwa mtazamo wa uchumi wa Kiislamu. Ifahamike uchumi wa nchi una mambo mengi ndani yake ikiwemo suala la Uzalishaji kupitia Kilimo, Viwanda na Utoaji huduma za msingi nakadhalika. Hivyo sekta ya fedha ni eneo dogo kwa uchambuzi lakini ni muhimu mno katika maendeleo ya uchumi wa nchi. Katika vipaumbele sita vya CCM vilivyoainishwa katika Muhtasari wa ilani, suala la uchumi linachukuwa 50% ya vipaumbele vyote kama vifuatavyo; 1. Kukuza uchumi wa kisasa, fungamanishi, jumuishi na shindani uliojengwa katika msingi wa viwanda, huduma za kiuchumi na miundombinu wezeshi; 2. Kuleta mageuzi ya kilimo, mifugo na uvuvi ili kuwa na uhakika wa chakula na kujitegemea kwa chakula wakati wote na kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya uchumi; 3. Kutengeneza ajira zisizopungua 8,000,000 (milioni nane) katika sekta rasmi na isiyo rasmi kwa ajili ya vijana. Kwa vipaumbele hivi, inaweza kusemwa kuwa ilani hii ni ya kukuza uchumi na maendeleo ya uchumi. SEKTA YA FEDHA Katika ukurasa wa 19 wa ilani, umuhimu wa sekta hii unatambuliwa. Ilani inasema "Kutokana na umuhimu wa sekta ya fedha katika kuchochea shughuli za kijamii na kiuchumi, katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2020, Chama kiliendelea kuisimamia Serikali kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha huduma za fedha kwa wananchi." Kadhalika katika ukurasa wa 213, ilani inasema "Huduma za fedha, ikiwemo za kibenki na mifumo ya malipo, masoko ya mitaji, bima, hifadhi za jamii, na huduma ndogo ndogo za fedha (microfinance), ndio mlizamu wa kuimarisha uchumi." Hivyo, huduma za fedha ni muhimu katika kuimarisha na kuharakisha miamala ya kiuchumi Katika awamu ijayo, Ilani imebainisha baadhi ya hatuwa ambazo zinastahili pongezi, nazo ni: Mosi, kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa gharama nafuu kwa kupanua wigo wa matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma za kifedha ili kuongeza huduma jumuishi za fedha nchini, kuchochea uwekezaji wa ndani na kukidhi mahitaji halisi ya wananchi hususan wa kipato cha chini na waishio vijijini. Pili, Kupunguza vikwazo vya ushirikishwaji wa Watanzania kwenye mfumo rasmi wa fedha, ikiwemo kuimarisha ulinzi wa watumiaji wa huduma za kifedha (consumer protection) kwa kukamilisha na kutekeleza Mpango Kabambe wa Taifa wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha 2019/20 - 2029/30. Tatu, Kuboresha na kuimarisha huduma za kifedha zikiwemo benki, masoko ya mitaji, bima na huduma ndogondogo za kifedha na utendaji wa taasisi za sekta ya fedha na kodi ili ziendelee kutoa mchango mkubwa katika ukuzaji wa uchumi wa Taifa. Taasisi hizo ni pamoja na Benki kuu ya Tanzania (BoT), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA). Nne, hususani kwa upande wa Zanzibar, ilani ya CCM ukurasa wa 214 (F) inaelekeza SMZ "Kuimarisha huduma za kifedha kwa mfumo wa uchumi wa Kiislam." Kwa upande wa pili, zipo hatuwa ambazo zinachukiza. Hatuwa hiyo ni ile ambayo imetajwa katika muhtasari wa ilani ukurasa wa 18 F (ii) kuwa katika kutengeneza ajira Milioni 8, mambo ambayo chama kinaahidi kufanya ni pamoja na " Kuwawezesha vijana kushiriki katika shughuli za ujasiriamali, ikiwemo kuwapatia mafunzo na kuwaunganisha na taasisi na asasi za utoaji mikopo yenye riba na masharti nafuu;" Ujasiriamali sawa, kupata mafunzo sawa lakini kuunganisha vijana wakiwemo vijana wa kiislam na taasisi za utoaji mikopo yenye riba, hili ni baya mno! Uislam unakataza kujihusisha na riba kwa kuwa ni dhambi kubwa na yenye kuangamiza duniani na akhera. Hii inatia doa ilani hii. MAPENDEKEZO. Kwa ujumla, napendekeza mambo yafuatayo yazingatiwe iwapo chama cha CCM kitaendeleya kuongoza serikali: 1. Kusahihisha dosari hii iliyopo katika muhtasari huu kwa kuahidi ya kwamba "itawaunganisha na asasi za utoaji mikopo yenye riba na ambayo haina riba!" Ni wajibu wa serikali, kuhakikisha taasisi na asasi zake kama mabenki ya serikali yanayohuduma ya mikopo bila riba kwa njia ya kufanya mauziano au kukodisha au ushirika katika faida na hasara na wateja wake. 2. Izingatiwe na watunga sera na mipango ya nchi kuwa kikwazo kikubwa cha ushirikishwaji wa Watanzannia kwenye mfumo rasmi wa fedha sio kukosekana ulinzi wa watumiaji wa huduma za kifedha (consumer protection) pekee bali kuachwa huduma za kibenki kutowa mikopo kwa njia ya RIBA, kuachwa taasisi za mikopo midogo kutoza RIBA, kuachwa huduma za bima kufanya shughuli zake kama mashirika ya kamari na kuwekeza kwa njia za RIBA, kukosekana ushirikishwaji wa taasisi za kijamii zenye wataalamu Waislam kutoka Bara kama vile CIFCA na kutoka Zanzibar kama vile UKUEM katika uandaaji wa Mipango ya Maendeleo ya Sekta ya Fedha. Kukosekana ushirikishwaji huu kumepelekeya watunga mipango kutozingatia desturi, mila na dini za wananchi ambao ndio walengwa wa mipango husika. Jambo hili linapaswa kusahihishwa haraka iwezekanavyo. 3. Ilani iweke wazi zaidi kile kinachokusidiwa kufanywa. Kwa mfano ilani inasema "Kuweka mazingira wezeshi kwa sekta ya bima kukua zaidi, kuwanufaisha wananchi wengi na kuchangia katika uchumi kwa kiwango kikubwa zaidi;" Ni mazingira gani hayo ambayo kwa sasa hayapo na hivyo yatawekwa ili sekta hii ikue zaidi? Ndani ya muda gani mazingira hayo yatakuwa yameshawekwa? Hivyo ni muhimu watunga ilani watusaidie kujibu maswali hayo bila kusahau kilio cha muda mrefu cha kuwa na bima ya Kiislamu (Takaful) ambayo kwa takribani miaka 5 yote imekosekana idhini ya waziri wa fedha bila kuwepo kwa sababu zozote zinazofahamika. 4. Kama ambavyo imeoneana umuhimu kwa upande wa Zanzibar kuimarisha huduma za kifedha kwa mfumo wa uchumi wa Kiislamu, kadhalika kwa upande wa bara umuhimu huo ni mkubwa zaidi ukinzingatia kuwa Waislam waliopo bara ni wengi zaidi ya waislam wote wa Zanzibar. Na mahala mnasaba pa kuanzia ni mpango kabambe wa maendeleo ya sekta ya fedha utambue mfumo wa fedha wa Kiislamu na taasisi za fedha zote za serikali na zile ambazo serikali ni mmiliki wa hisa nyingi, kuwe na mipango ya makusudi ya kuanzishwa huduma za kifedha zinazokidhi mfumo wa uchumi wa Kiislamu. Iwapo dosari hizi zitarekebishwa na kutekelezwa, ni matumaini yangu serikali itafanikiwa katika vipaumbele vyake vitatu vya kiuchumi vilivyoainishwa hapo juu kwa maslahi ya wote na sio kwa maslahi ya wachache.

Wednesday, August 26, 2020

JENGA UCHUMI WAKO BINAFSI

Tumezoea kusikia kuhusu kujenga uchumi wa nchi na kuleta maendeleo. Tunaambiwa kuwa uchumi unakuwa kila mwaka na hivyo maisha ya watu yanaimarika. Hali hiyo inaweza kuwa sahihi iwapo wewe na mimi tunajizatiti kujenga uchumi wetu binafsi. Na abadan ukuaji huo wa uchumi hautomnufaisha yule ambaye amekaa maskani asubuhi na jioni akizungumza kuhusu mechi au wanayosema wanasiasa majukwaani au wanayofanya wasanii au amekaa nyumbani na kutazama filamu mbalimbali au kucheza games za kieletroniki n.k Hivyo, ili uchumi wako binafsi uimarike lazima kila mmoja wetu ajizatiti katika mambo yafuatayo muda wote wa uhai wake. 1. Ajifunze misingi ya elimu ya biashara. Iwe mfanyabiashara au mfanyakazi, elimu ya biashara ni elimu muhimu sana kwa kila mmoja wetu. Unatakiwa ujuwe biashara ni nini? Namna ya kuweka mahesabu, namna ya kuuza bidhaa au huduma, namna ya kuzungumza na wateja, namna ya kupata mitaji, namna ya kujitangaza na namna ya kuibuwa mawazo ya kibiashara ambayo yatatatuwa tatizo la mtu au watu kwa njia ambayo watu hao watakauwa tayari kulipiya ili kupata ufumbuzi wako. Somo la biashara hufunzwa katika elimu sekondari kupitiya somo la commerce na book keeping. Kwa bahati mbaya, watu wanahiyari ya kuyawacha masomo hayo wanapoingiya kidato cha tatu. Kwa maoni yangu, ilipaswa kuwe na somo moja mjumuiko wa masomo haya ambayo iwe mtu ni wa arts au science ataendeleya kusoma ili kumjenga kujuwa namna biashara inavyopaswa kufanywa. Umuhimu wa somo hili ni kuhakikisha ya kwamba anayemaliza kidato cha nne awe anayomsingi imara wa kuweza kujiajiri na kujenga uchumi wake na wa familiya yake. Biashara tunazofanya kimazoea na kupitia ushauri wa rafiki badala ya wataalamu, hautoshi kukuimarisha kiuchumi. Hata ikiwa ulipitwa na masomo hayo, sasa hivi katika umri ulionao tenga muda wa kusoma maudhui fulani za somo la biashara na ufanyie kazi. Hatuwa hizi zitakuweka katika mstari wa kujenga uchumi wako. Soma sana vitabu au sikiza mazungumzo yanyolenga kukuongozea maarifa katika ufanyaji biashara iweya vitu au ya kutoa huduma (mwajiriwa) 2.Tumia muda wako vizuri. Muda ndio rasilimali kubwa aliyopewa mwanadamu na neema kubwa kabisa ni kuwa na imani/ tawheed. Kama muislam, ushapewa neema ya tawheed na kinachofuata ni kutumia rasilimali ya wakati vizuri. Wakati ndio uhai wenyewe. Ukitoka kazini au ukishafunga biashara yako jioni, jiulize maswali yafuatayo; kitu gani napaswa kufanya ili kuboresha utendaji wangu kazini au kuboresha biashara yangu? Watu wengi huwa hawana jawabu ya swali hili. Hiyo sio dosari. Dosari ni kuridhika kwa kukosa jawabu! Dosari ni kudhani kuwa hamna anayejuwa jawabu! Dosari ni kuifungiya ndani ya fikra zako na ukawacha mlango wa kutafuta ushauri kwa wengine. Imesemwa "washauri wenye ujuzi, utapata nuru ya maarifa yao." Hivyo badala ya kupoteza muda wako wa jioni ukishafunga kazi au kupoteza muda siku za week end, tumiya muda huo kujumuika na familiya yako na piya kukusanya maarifa mapya ili kuboresha zaidi. Hili ni jukumu lako la kila siku ili kujenga uchumi wako ambao utakuwa imara. 3. Weka malengo yako na ujilazimishe kuyatimiza. Ni muhimu uwe na malengo ya kukuza kipato chako kila mwaka. Iwe kwa kupitiya ajira au kwa kulima au kwa kuzalisha au kwa kufanya biashara ambazo zinaboresha maisha ya watu wengine. Tunaishi wakati ambo taarifa za watu wengine ni nyingi mno katika magazeti, mitandaoni na mitangazo. Taarifa hizi nyingine zinaweza kukupa maarifa na nyingine zinaweza kukutowa katika malengo yako. Hivyo ni muhimu ujilazimishe kuyafikiya malengo yako kila mwaka na usikubali kuondoka katika malengo uliyojiwekeya na kuishi katika malengo ya wengine. Sasa tupo katika mwaka mpya wa Kiislam, chukuwa kalamu na karatazi uandike kipato ambacho ungependa ukifikiye ifikapo mwisho wa mwaka na nini unapaswa kufanya ili kufikiya malengo hayo. Usipofanya hivyo, usilalamike pale gharama za maisha zinapoongezeka na wewe miaka nenda rudi umejifunga katika kipato cha miaka ya nyuma! Kila siku zinavyoenda unatakiwa ujenge uchumi wako au hali ya kiuchumi itakuwa na changamoto ya kutegemeya wengine. Weka malengo na kisha tekeleza peke yako au pamoja na wengine!

Wednesday, August 19, 2020

MATATIZO YA KIUCHUMI (ECONOMIC PROBLEM)

Nchi zote duniani hufanya juhudi kubwa katika kujenga uchumi imara na maendeleo kwa watu wake. Nimeeleza katika makala iliyopita mitazamo miwili tofauti kuhusu suala la maendeleo. Kujenga uchumi imara na kuleta maendeleo iwe kwa misingi ya kiislam au vinginevyo ni kazi ngumu na yenye kuhitaji umakini mkubwa kwa upande wa viongozi na wanaoongozwa. Si jambo la viongozi pekee kusema hiki na hiki tunachofanya ndio maendeleo au ndio ukuaji wa uchumi. Ikitokeya hivyo, wananchi wana kila sababu ya kuhoji aina hiyo ya maendeleo inayosemwa na viongozi wao. Na jambo hili limekuwa likijitokeza mara kadhaa kwa sababu mbili; Ya kwanza, kukosekana ushirikishwaji wa wananchi katika majadiliano ya maendeleo wayatakayo na uchumi imara wanaoutaka (lack of public participation). Je watendaji wa serikali wanakusanya maoni yetu na kuyafanyia kazi? Ya pili, tabiya ya viongozi na wanasiasa kuhodhi maamuzi ya matumizi ya rasilimali mbalimbali katika maeneo yao (dominance of political elite in decision making on resource utilization). Mambo haya yanahitaji kusahihishwa. Ili kufanikiwa katika usahihishaji wa mambo haya, tunahitaji kujiuliza tatizo au matatizo ya kiuchumi yanayowakabili watu wetu ni ya sampuli gani? Wachumi kama Lionel Robins waona kuwa tatizo la kiuchumi la watu wetu chanzo chake ni uhaba wa rasilimali (scarcity of resources). Wanamahitaji mengi lakini rasilimali ni chache ili kukidhi mahitaji hayo. Kwa upande wa wachumi wa Kiislam, tatizo la kiuchumi linalowakabili watu wetu linachukuwa sura zifuatazo: 1. KUKOSEKANA KWA FURSA SAWA (EQUAL OPPORTUNITIES). Binadamu ni viumbe vya Allah na wote wanahadhi kwa ubinadamu wao. Wote wana mahitaji sawa ya msingi katika kuendesha maisha yao ya kila siku. Wanahitaji kula, kunywa, kupata elimu, kupata ajira, kupata matibabu, kupata fursa za kujiongezeya mapato, kugombeya nafasi za uongozi, kutowa maoni na ushauri, kudai haki katika vyombo vya sheria n.k. Tatizo la kiuchumi kwa watu wetu hujitokeza pale mamlaka fulani haitowi fursa sawa kwa watu wote kujipatia mahitaji yao. Tulieleza wiki iliyopita mifano kadhaa kuhusu fursa za mikopo kutoka Baraza la Uwezeshaji Kiuchumi ambazo haziwapi fursa waislam kunufaika kutokana na uwepo wa Riba katika mikopo hiyo pamoja na kuwa sehemu ya fedha zao ndio zinazoendesha mifuko hiyo kwa kupitiya kodi mbalimbali. Katika fursa za ajira serikalini, sauti za waislam wamekuwa zinalalamika kuwa ni waislam wachache mno wanaopewa fursa hizo. Kadhalika katika fursa za elimu ya juu, kuna malalamiko kuwa waislam ni mdogo kuliko wa dini nyingine. Kwa ujumla inapotokeya kuwa watu hawana fursa sawa za kujipatiya mahitaji yao, hili ni tatizo ambalo linahitaji umakini mkubwa kulitatuwa na inawezekana. Sio mambo ya kupuuza bali kuyafanyia kazi kwa umakini mkubwa. 2. UBORA WA MAISHA ( QUALITY OF LIFE). Binadamu kwa uhalisia wake ni mjumuiko wa kiwiliwili na roho. Hivyo, ubora wa maisha ya binadamu upo katika kujengewa uwezo wa kiimani (spiritual) na uwezo wa kuyamudu mazingira yake (materials). Tatizo la kiuchumi lipo katika kutafuta njia maridhawa zenye kuweka uwiano baina ya mambo haya mawili ili binadamu huyu aweze kufikiya kilele cha kuwa na utu na vitu. Sera za kiuchumi zenye kujenga fursa za kuwa na vitu zinapelekeya watu kuwa mtu-vitu (materialist). Athari yake ni kuwa na ongezeko la wizi, ongezeko la rushwa, ongezeko la dhuluma n.k Na sera zenye kujenga fursa za kuwa na imani zinapelekeya kuwa na watu waliojitenga na ulimwengu wao (spiritualist). Athari yake ni kuwa na watu wanaojitenga na kufanya kazi n.k Mambo haya mawili yanahitajika kwa binadamu ili kuwa kamilifu kama alivyoumbwa na Mola wake, awe na utu na vitu kwa ustawi wa ubinadamu na mahitaji yake. 3. UADILIFU NA HAKI. Tatizo la mwisho la kiuchumi kwa mtazamo wa Kiislamu ni namna gani ya kumlinda mtu mwenye rasilimali yake iwe kipawa, maarifa au kitu dhidi ya wale ambao wanataka kumnyonya au kumpokonya au kumdhulumu jambo ambalo mwisho wako litaathiri ubora wa maisha yake na kukosekana kwa fursa baina ya wananchi. Kwa mfano, kuna wananchi wengi mno ambao wanamiliki ardhi lakini hawana hati miliki za viwanja hivyo. Wapo katika hali ya hatari inayoweza kupelekeya kupoteza mali zao kwa kudhulumiwa na wananchi wenzao au hata na watumishi wa serikali wasiokuwa waadilifu. Mfano wa pili ni utaratibu wa kuwa ardhi yote ni ya serikali na mwenye hati amekodi tu (leasehold) unaweza kuwaweka wananchi wengi katika hatari ya kupoteza mali zao baada ya muda wa kukodi kuisha (lease) na ikawa yule aliyekodishwa au mwenye hati hiyo hakuomba kuendeleya kuikodisha ardhi hiyo (lease renewal) ndani ya muda uliowekwa. Jambo hili sio la kufikirika bali yametokeya kwa baadhi ya wananchi wa Kenya ambao walijikuta nyumba zao zikibomolewa katika mji wa Nairobi na wamiliki wapya kwa kuwa hawakurenew hati zao! Wakati huo huo baadhi ya wananchi wenzao hati zao ni za kudumu na sio kukodishwa (freehold). Kwa upande wa pili, ni tatizo la kiuchumi na kijamii iwapo sheria zetu hazikidhi aina mbalimbali za miamala au ufanyaji wa biashara. Kwa mfano biashara ya bima ya Kiislam, sheria na kanuni zilizopo hazikidhi matakwa ya biashara hiyo na kuwa kanuni mpya zinahitajika. Ukosefu wa kanunni hizo mpya zimepelekeya kukosekana bima ya kiislam nchini Tanzania. Hivyo baadhi ya wananchi wananufaika na huduma za bima na kulipwa fidia wakati wa majanga na sehemu ya wananchi wanakoseshwa kupata huduma hiyo kwa sababu ya msingi-nayo ni kuwa bima zilizopo zinaenda kinyume na mafunzo ya dini yao! Kwa upande mwingine, sheria zenye kuingiliya haki ya umiliki mali zinahitaji mabadiliko. Kwa upande wa vyombo vya mahakama lazima viwe uwezo mkubwa wa kusikiliza kesi kwa wakati na haraka ili kila mwenye haki yake aweze kuipata na kunufaika. Hivyo, ni suala la msingi kuwa sera, sheria na vyombo vya mahakama vinasimama katika uadilifu na haki. Mwenyezi Mungu anasema "Enyi mlio amini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu...(4:135). Kwa kuhitimisha, matatizo yetu ya kiuchumi si uhaba wa rasilimali peke na wingi wa mahitaji peke yake bali pia ukosefu wa fursa sawa, ubora wa maisha yenye uwiano baina ya utu na vitu na ukosefu wa uadilifu na haki.

Wednesday, August 12, 2020

UCHUMI JUMUISHI NA MCHANGO WA CIFCA

Wiki iliyopita tulitowa mfano mmoja unaonesha upungufu wetu katika kujenga uchumi jumuishi. Makala haya yataeleza mifano mingine michache na kueleza mchango wa CIFCA katika masuala ya fedha na kuwa na uchumi jumuishi. Mikopo wa wafanyakazi serikalini. Serikali kama taasisi nyingine hutowa mikopo nafuu kwa watumishi wake. Mikopo hiyo huelezwa kuwa haina riba lakini kwa jicho la Uislam ipo riba iliyojificha au kufichwa chini ya kile kinachoitwa tozo mbalimbali za mkopo huo. Wanachuoni wanaona kuwa mkopo wowote ambao unatozo au unamnufaisha mkopeshaji isipokuwa tozo halisi tu ambazo hulipwa kwa watowa huduma wengine. Kwa mfano tozo ya kutuma mkopo kwenye simu au kwenye bank yako inaweza kukusanywa na mkopeshaji kama gharama halisi ya mkopo unaotolewa. Gharama au tozo ambazo hazifungamani moja kwa moja na gharama halisi za mkopo. Baraza la Taifa la uwezeshaji wananachi Kiuchumi (NEEC). Baraza la taifa ambalo limeundwa na kuanza shughuli zake mwaka 2005 lina dhima ifuatayo "Kuongoza Watanzania kuelekea katika uchumi thabiti wa taifa kwa kutengeneza mazingira rafiki ya biashara na ushiriki sawa katika kiuchumi." Ni dhima inayoleta matumaini na baraza lina program nzuri za kuwawezesha watanzania kujiimarisha kiuchumi. Hatahivyo, yapo maeneo machache yanayopaswa kufanyiwa kazi ili kuwapa waislamu fursa sawa na wananchi wengine. Tovuti ya baraza inaeleza kuwa kuna mifuko ya Serikali na Programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi 45 ambazo zinaratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi. Makala haya haitoweza kuangalia mifuko yote hiyo bali tutatazama mifuko inayohusiana na utoaji mikopo moja kwa moja kwa wajasiriamali kwa mfano; 1. Mfuko wa Rais wa Kujitegemea (Presidetial Trust Fund –PTF). Mfuko unatowa mafunzo, mikopo na kufanya tafiti. Ni wazo zuri sana kuwa na mfuko namna hii hata hivyo huduma yake ya mikopo inaweza ikawa sio jumuishi au rafiki kwa waislam iwapo kuna riba ndani yake. Tovuti ya mfuko kwa sasa inaonesha aina za mikopo, masharti na kiwango cha mikopo lakini ipo kimya kuhusu tozo au riba yoyote inayotozwa na mfuko. Suali muhimu ni je mfuko huu unatozza riba kwa mikopo yake au la? Ikiwa inatoza basi ni wazi kuwa sio rafiki kwa waislam kwa kuwa kwa waislam riba imekatazwa. Ikiwa hamna riba, hii itakuwa ni mfano mmoja unaodhihirisha kuwa inawezekana kutowa mikopo bila riba na hivyo harakati za mfuko zinahitaji kupongezwa kwa kuwa jumuishi. 2. Mfuko wa Maendeleo ya Vijana (Youth Development Fund –YDF), Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (Women Development Fund –WDF) na Mfuko wa Taifa wa Kuendeleza Wajasiriamali Wananchi(National Entrepreneurship Development Fund –NEDF). Kimsingi fikra ya kuwa na mifuko hii ni nzuri mno. Hatahivyo, mikopo yake hutolewa bila riba? Ikiwa ni mikopo yenye riba au tozo, hiyo ni mushkeli mkubwa kwa waislam na hivyo kutonufaika ipasavyo na mifuko hiyo. Changamoto na tatizo la riba lipo katika mifuko mingine inayoratibiwa na baraza. Kadhalika, baraza katika utekelezaji wa majukumu yake linaweza kutowa mkopo kwa mtu au shirika kwa mujibu wa masharti waliyojiwekeya. Je mikopo hiyo ina riba au la? Kimsingi, baraza katika kutekeleza majukumu yake ni muhimu mno kuzingatia ujumuishi wa taratibu za mikopo ili baraza hili liwe na manufaa wa watu wote. MCHANGO WA CIFCA Waislam baada ya kutambuwa changamoto zilizopo katika sekta ya fedha na uchumi, waliaamuwa kuanzisha chombo chao chenye lengo la kushauri na kufunza yoyote yule ambaye angependeleya kufuata mfumo wa fedha na uchumi usiohusisha suala la riba. Kadhalika, chombo hicho kinaendeleya kutowa elimu kwa waislam juu ya tatizo la riba katika mikopo mbalimbali ikiwa na lengo la kuhadharisha na kuonesha njia mbadala. Hivyo, ni muhimu sana hususani sekta ya umma kushirikiana na chombo hiki nchini ili mikopo inayotolewa na taasisi za serikali na mifuko ya baraza la taifa iweze kunufaika na wataalamu bobezi wa masuala ya fedha na uchumi waliopo katika chombo hicho na hivyo kuongeza kasi juhudi za baraza. Itambulike ya kwamba, taratibu zisizo na riba ni jumuishi kwa kila mtanzania na sio kwa manufaa ya waislam peke yao. Kadhalika nitoe wito kwa taasisi binafsi za fedha na utoaji mikopo, kutambuwa kuwa lipo kundi kubwa la watanzania ambao hawafurahishwi na hawaridhii miamala ya riba kabisa na sio suala la riba kubwa au ndogo. Riba yote iwe ndogo au kubwa, haifai. Kwa rehema zake Mola ametuwekeya njia nyingi ambazo zinaiwezesha taasisi kufanya biashara na kupata faida isiyokuwa riba. Hivyo, wachukuwe fursa inayopatikana kwa kuwepo kwa CIFCA nchini ili kuweza kushauriwa namna ya kufanya ili waweze miamala sahahi na kutowa huduma zisizokuwa na riba kwa manufaa ya watanzania wote. Jambo hili linawezekana iwapo taasisi husika itakuwa na utashi thabiti na kufuata maelekezo ya wataalamu wa CIFCA katika kuepukana na Riba pamoja na vipengele vingine ambavyo ni vya kinyonyaji.

Wednesday, August 5, 2020

UCHUMI JUMUISHI

Maendeleo ya kiuchumi ni eneo muhimu baada ya yale ambayo tuliyaeleza wiki iliyopita. Katika hotuba ya bajeti ya wizara ya fedha mwaka huu, Waziri wa Fedha alibainisha dhamira ya serikali kuwaleteya wananchi maendeleo ya kiuchumi na kuwajumuisha wananchi katika maendeleo ya kiuchumi. Mikakati kadhaa kila mwaka huwekwa ili kufikiya azma hii. Katika yale ambayo Waziri alibainisha kwa mfano ni kufutwa kwa ada na tozo za kero ili kuboresha mazingira ya kufanya biashara na kuwekeza hapa nchini. Uwekezaji katika miundombinu wezeshi kwa shughuli za uzalishaji mali na biashara ili kukuza uchumi, kuendelea kuorodhesha Hatifungani zake katika Soko la Hisa la Dar es Salaam; na kutoa elimu kwa umma ili kuhamasisha ushiriki wao katika kuwekeza kwenye Hatifungani na Dhamana za Serikali, kusimamia na kuboresha sekta ya fedha; kuongeza upatikanaji wa huduma za msingi kama vile afya, elimu, maji na umeme hususan maeneo ya vijijini; na kuendelea kutekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) ili kuongeza kipato chao na kuwawezesha kupata mahitaji ya msingi na kadhalika. Je mikakati hii inawapa fursa sawa wananchi kujumuika kwa katika kuziendea fursa za uchumi? Jawabu ni ndio na hapana! Ili kufahamu hoja za jawabu hii kwanza tujiulize ni nini uchumi jumuishi ambao wachumi katika karne hii wanaona kuwa ni njia muwafaka ya kuhakikisha uchumi unakuwa vizuri na kuwa imara. UCHUMI JUMUISHI (INCLUSIVE ECONOMY). Ukiwauliza watu wa kawaida nini uchumi jumuishi watakuwa na jawabu tofauti na hilo pia lipo kwa upande wa wachumi. Wapo wanaona kuwa uchumi jumuishi ni ule ambao watu wanafursa sawa ya kupata ajira yenye hadhi na kipato halali. Ni uchumi ambao kila mwananchi anahusishwa katika fursa zilizopo za kupata kipato na anaweza kuziendeya fursa hizo bila kikwazo chochote iwe dini au kabila au eneo alilopo na kadhilika. Ni uchumi ambao fursa haziwapendelei watu fulani tu iwe kwa utajiri wao au kwa dini zao au kwa uanachama wao nakadhalika bali kila mtu anaweza kunufaika kikamilifu na fursa zilizopo. Tafsiri moja wapo ambayo inanivutiya zaidi ni ile inayosema kuwa uchumi jumuishi ni ule ambao unawajali watu wote kwa mujibu wa mitazamo yao ya kiuchumi ( inclusive economy as the one that support all people from their economic standpoint). Baada ya kufahamu maana ya uchumi jumuishi, je hatuwa hizi zilizoainishwa na Waziri ni hatuwa zenye kujenga uchumi jumuishi? SIFA YA UCHUMI JUMUISHI NA HALI YETU. Wachumi wamebainisha vigezo au sifa kadhaa za uchumi jumuishi kama vile; ushiriki wa wananchi (participation), usawa wa fursa mbalimbali (equity), kuongezeka kwa mapato (growth), endelevu (sustainable) na imara (stability). Ukitazama sifa hizi na ukilinganisha na hatuwa ambazo waziri amezibainisha utaona kuwa zipo ambazo zimekidhi sifa hizo kama vile kufuta ada na tozo zenye kero, kuwekeza katika miundombinu, upatikanaji wa huduma za msingi,kunusuru kaya masikini na kadhalika. Na kwa upande mwingine, kwa mtazamo wa kiuchumi wa kiislamu, baadhi ya hatuwa zilizotajwa sio jumuishi kikamilifu na hazitowi fursa sawa kwa wote. Kwa mfano, kuoridhesha hatifungani na dhamana za serikali zinazolipa riba. HATIFUNGANI NA DHAMANA ZA SERIKALI. Waziri amesisitiza kuwa serikali itatowa elimu kwa umma ili kuhamasisha ushiriki wao katika au kununuwa au kuwekeza kwenye Hatifungani na Dhamana za Serikali. Kimsingi, serikali huhitaji fedha kwa ajili ya shughuli zake mbalimbali za kuwatumikiya wananchi. Na njia moja maridhawa ni kufanya biashara na wananchi wao, kwa maana ya kuwataka wawekeze katika hatifungani na dhamana zake ili wapate faida na kuongeza kipato chao na huku fedha hizo zinaenda katika kuimarisha miundombinu au huduma muhimu kwa wananchi. Hivyo wananchi wananufaika pande zote mbili. Dosari iliyopo kwa mtazamo wa Uchumi wa Kiislamu ni kuwa hatifungani na dhamana za serikali zimetengezwa katika muundo ambao serikali wanauza hela kwa hela au kitaalamu inakopa kwa wananchi wake na kuwalipa na riba (interest). Hapa kuna tatizo la muundo (structural fault). Nini tatizo? Muundo huu unawanyima na kuwakosesha fursa sawa sehemu ya wananchi hususani waislamu katika kushiriki katika kufanya uwekezaji kwa kupitiya serikali yao kwa kuwa wao, HAWARUHUSIWI kukopa au kukopesha kwa riba au kuuza hela au kukodisha hela kwa hela! Riba ni dhambi kubwa sana katika Uislamu. Ubaya wake umefananishwa na kutangaza vita na Mwenyezi Mungu au kufanya tendo la ndoa na mama yako mzazi. Anayekula riba ataingiya motoni isipokuwa atakapo tubiya na kuachana na riba. Kwa kutolifahamu jambo hili, serikali sio tu haitoweza kupata fedha za kutosha kutoka Waislam wanaofuata dini yao na Waislamu hawatoweza kupata kipato cha ziada. Hivyo, serikali inaumiya na wananchi hawa wanakosa fursa ambayo wenzao wengine wanaipata! Lakini baya zaidi ni kuwa, serikali inapolipa riba kwa wale ambao watawekeza katika hatifungani na dhamana hizo kwa kuwa dini zao haziwazuii kukopesha kwa riba itakuwa inatumiya kodi zetu sote kuwanufaisha kwa malipo ya riba baadhi tu ya wananchi! Hali hii inadhihirisha wazi kuwa muundo wa serikali wa kukopa kwa riba kwa kuuza hatifungani na dhamana (Treasury bills and treasury bonds), sio jumuishi kwa wananchi wote. Ni muundo unaowabaguwa waislamu kwa kuwafanya wasishiriki katika kufanya 'biashara' serikali na kupata faida ya halali. Ni muundo ambao inahitaji kufikiriwa upya ili kutafuta muundo mwingine ambao utaiwezesha serikali kupata hela au kukidhi mahitaji yake na wananchi kuwekeza na kupata faida halali. je ipo njia mbadala? NINI CHA KUFANYA? Njia tulioieleza hapo awali ya kukopa kwa riba ni kongwe na imekuwa ni ya mazoeya lakini ukweli ni kuwa sio shirikishi kwa wananchi wote na ni yenye kubaguwa waislamu. Wachumi wa Kiislamu, wameshapendekeza miundo mengine ambayo serikali inaweza kupata hela au ukidhi mahitaji yake bila ya kutumiya mkataba wa kukopa kwa riba na badala yake kutumiya mikataba mingine kama vile ya mauziano (sales) au kukodisha (leasing) au kushirikiana katika faida na hasara (partnership). Jina maarufu la njia zenye kufuata mikataba hii ni Sukuk. Zipo Sukuk aina nyingi na zenye kuundwa kwa mikataba mbalimbali lakini sio mkataba wa kukopa (loans contract). Njia hii y Sukuk, imeshatumika nchi kadhaa ikiwemo Afrika Kusini, Nigeria, Gambia, Senegal, Sudan na nchi nyingine. Miundo hii (Sukuk) inayowafikiana na kanuni za kibiashara za Kiislamu hazibagui watu wa dini nyingine kwa kuwa hazipingani na mafunzo ya dini hizo. Waislamu na wasiokuwa waislamu wanaweza kushiriki kwa usawa. Je njia hizo zinawezesha wananchi kupata faida? Ndio. Kwa mfano, serikali inataka fedha kwa ajili ya kununuwa mitambo ya Umeme wa Stigler's Gorge ili kuzalisha umeme nchini. Ili kukidhi haja hii serikali kwa kupitiya bank kuu inakaribisha wananchi kuchanga fedha ambazo zitatumika kununuwa mitambo hiyo kwa bilioni 100 kwa mfano, na serikali itaahidi kununuwa mitambo hiyo kutoka kwa wananchi kwa Bil 105 na wananchi hao watalipwa ndani ya mwaka au miaka mitatu na kadhalika kulingana na kila mmoja alivyochangiya na gawio la faida. Kwa utaratibu huu, haya ni mauziano kwa faida na sio kukopeshana. Hii ni biashara halali ya mali kwa fedha na sio biashara haramu ya fedha kwa fedha. Hii ni njia moja tu katika njia nyingi zilizobuniwa na wachumi waislam katika kuiwezesha serikali kupata mahitaji yake (financing government deficit budget) ambayo waislam na wananchi wote kwa usawa wanaweza kushiriki na kuhimizana kushiriki kikamilifu na kuiondoleya serikali kazi ya ziada katika kuhamasisha. Hivyo, jambo hili linawezekana na wapo wataalamu wa kutosha duniani wa kuishauri serikali katika kuweka muundo ambao unaepukana na riba. Kinyume na hivi, waislam wanasikitika mno kuona matangazo ya serikali yanahamasisha kununuwa hatifungani na dhamana zake kwa njia ya riba ilhali zipo njia mbadala zisizo na riba ambazo na wao wanaweza kushiriki bila kuvunja kanuni za dini yao. Waislamu wanahuzunika kuona serikali itatumiya kodi zao kulipa riba kwa baadhi ya wananchi na kuwanufaisha watu wachache tu. Ili kutuondoleya masikitiko haya na huzuni hizi, tunaiomba kwa heshima kubwa serikali yetu sikivu ione kuwa kuna haja sasa ya kubuni njia mbadala ambazo zitawapa wananchi wote fursa sawa ya kushiriki katika kuiwezesha serikali kupata mahitaji yake na wananchi kupata fursa ya kupata kipato cha halali.

Wednesday, July 29, 2020

MAENDELEO TUYATAKAYO


Tupo katika mwaka wa uchaguzi mkuu wa nchi nzima. Vyama mbalimbali vitarudi kwa wananchi kunadi sera zao na mipango yao ya kuwaleteya wananchi maendeleo. Je ni maendeleo gani tuyatakayo watanzania na waislamu?

Dhana ya Maendeleo.

Neno hili "Maendeleo" (Development), hupendwa sana kutumiwa na wanasiasa wanapojinadi kwa wananchi. Wataalamu wa lugha ya Kiingereza wanasema kuwa neno hili "development" lilianza kutumika katika kuelezeya hatua za ukuaji wa viumbe katika miaka ya 1756. Na limekuja kutumiwa na wachumi katika miaka ya 1902 na kuendeleya likimaanisha kuwa ni hali ya kupiga hatuwa za kiuchumi (state of economic advancement). Dhana hii ya maendeleo ya kiuchumi ilishika kasi zaidi baada ya vita vya pili vya dunia na mijadala kadhaa ikifanyika mpaka kuja kuibuka kwa somo maalum liitwao "development economics." ambalo hufunzwa katika vyuo vikuu mbali mbali ulimwenguni.

Kimsingi kuna tafsiri nyingi sana kutoka kwa wachumi kuhusiana na swali hili, "maendeleo" ni kitu gani? Wengi wetu neno maendeleo tunalihusisha tu na weingi wa fedha, hali nzuri ya maisha inayomwezesha mtu kuweza kujikimu bila hofu, kuwa na miundombinu imara kama vile barabara, maji, shule, umeme, vituo vya afya, kukuza uchumi ili kutowa ajira nyingi nakadhalika. Mara nyingi viongozi na wanasiasa hukusudiya maana hii wanaposimama kujinadi majukwaani kuomba kura. Haya ni sehemu moja tu ya maendeleo.

Maendeleo katika Uislam.

Wachumi wa Kiislamu wamefanya kazi kubwa katika kubainisha mtazamo wa Uislamu kuhusu maendeleo. Pamoja na kuwepo mitazamo mbalimbali, wanachuoni hawa wanaona kuwa maendelo ni lazima yajumuishe na yahusishe maeneo matatu muhimu na makubwa. La kwanza, uwepo wa fursa kwa wote na uhuru wa mtu binafsi kujiendeleza mwenyewe bila hofu wala upendeleo (individual human self-development without fear or favour).Pili, uwepo wa mazingira rafiki na bora yenye kumwezesha mtu kufikiya malengo yake kipindi chote (physical and material development of the earth). Na la tatu, kuwepo kwa haya mawili kwa watu wote katika jamii husika (development of society as whole). Uislam unaona kuwa eneo la kwanza ni muhimu zaidi na ndio chachu ya kupatikana maendeleo katika maeneo haya mengine. Anasema Mchumi mmoa wa Kiislam Profesa Abdul Hamid Abdul Aziz "Mazingira ya mwanadamu yaandaliwe kutowa fursa na uhuru wa kubadilika kutoka hatuwa moja kwenda hatuwa iliyobora zaidi sio kimali tu na bali na kiimani na muruwa mwema (material and spiritual development)."

Uislam unaona maendeleo yoyote yale lazima yamwezeshe Mtu ambaye ni Khalifa wa Mwenyezi Mungu, aweze kutoka katika umasikini wa kipato, fikra, imani na utamaduni na kueleya katika mabadiliko ambayo yatamwezesha kuwa na utajiri wa maarifa, wingi wa Imani kwa Muumba wake, muruwa mwema au tabia njema, fikra madhubuti za kielimu na kuyamudu mazingira yake muda wote. Mtu huyu awe anajitambuwa mwenyewe, anatambuwa lengo la kuumbwa kwake, anamtambuwa Muumba wake, na majukumu aliyopewa kama Khalifa wa Mwenyezi Mungu ambayo yanalengo la kumtowa katika upotofu na giza na kumwingiza katika nuru na uongofu. Kwa lugha ya Qur'an hawa ndio Ar Rashidun (walioongoka na walioendeleya)

Maendeleo katika sura hii ndio ambayo Quran inayaona kuwa ni fadhila na neema kubwa pale Mola aliposema "Lakini Mwenyezi Mungu amekupendezeeni Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu, na amekufanyeni muuchukie ukafiri, na upotovu, na uasi. Hao ndio walio ongoka (walioendeleya).Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na neema zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima (49:7-8). Mtume salallahu alayhi wasallam amesema " Amefaulu (katika kila jambo) yule ambaye ni Muislam wa kweli aliyejisalimisha katika uongofu wa Mola wake, akaruzukiwa rizki yenye kumtosheleza mahitaji yake katika maisha ya Ulimwengu na Moyo wake ukawa wenye kushukuru na kukinai (usiokuwa na pupa na vitu au anasa za kilimwengu)." Vile Mtume s.a.w amesema " Sifa nne mwenye kuwa nazo, basi asiwe na hofu juu ya lolote alilolikosa ulimwenguni. Ya kwanza, Uaminifu (trustworthy) (dhana pana sana yenye kujumuisha kuwa Mwaminifu juu ya amri za Mola wako na juu ya yale uliyoaminiwa na viumbe wenzio iwe siri, kazi, au mali n.k). Ya pili, Ukweli (truthful) katika kauli zako na matendo yako ya kila siku, humdanganyi mtu wala huthubutu kumdanganya Muumba wako. Ya tatu, kuwa na tabiya njema zenye kupendeza hata watu wakawa hawaudhiki kwa kuwepo kwako pamoja nao, ikawa mfano wako ni sawa na mtende wenye kutowa mazuri zaidi kuliko unayochukuwa kutoka katika ardhi na kwa watu na ya mwisho, mwenye kutosheka na chakula chako cha kila siku." [Imepokewa na Imam Ahmad katika Musnad Ahmad].

Pamoja na hayo, Uislam umempa jukumu mwanadamu aindeleze ardhi au ulimwengu na mazingira yanayomzunguka kwa kumtaka awe Mus-liheeena (mwenye kufanya wema) na sio Mufsideena (mwenye kuharibu). Mola anasema "Na utafute, kwa aliyo kupa Mwenyezi Mungu, makaazi ya Akhera. Wala usisahau fungu lako la dunia. Nawe fanya wema kama Mwenyezi Mungu alivyo kufanyia wema wewe. Wala usitafute kufanya ufisadi katika ardhi. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi mafisadi." (28:77).

Maendeleo Tuyatakayo.

Kwa kuzingatiya kuwa dhana ya maendeleo ni mada pana mno Kiuchumi na katika Uislam na ambayo makala haya haitoshi kuijadili kwa urefu wake bali kukumbusha tu Waislam na wasomaji wafahamu Uislam una mtazamo wake na mafundisho yake yanalenga kumleteya maendeleo mwanadamu katika maeneo yake yote muhimu; kiimani, kiakili, kitabiya, kimali, kiafya na kimaisha kwa ujumla wake na sio kama nadharia za kimagharibi ambazo zimechukuwa baadhi ya mambo haya na kuyaacha mengine. Hivyo maendeleo tuyakayo ni lazima yajikite katika ujumuifu mambo haya yote na katika kuelezea nukta hii nitatowa mifano miwili tu.

Maendeleo ya Kiimani.

Mwanadamu anahitajio la kuamini katika maisha yake. Kwa kuwa hili halimwepuki, anaweza kuishiya kuamini ipasavyo au kupoteya katika imani yake hiyo. Na haiwezekani bali ni ujuha uliofurutu ada kuwa mwanadamu anaweza kudai yeye hana anachoamini. Hivyo binadamu anahitaji maendeleo ya kiroho na kiimani (spiritual development). Je kama taifa tunamjengeya imani gani mwananchi wa Tanzania? Ukitazama vyama mbalimbali, utaona kuwa vyama hivyo vina ambayo vinayaamini kwa mfano kipo chama kinachoamini kuwa "Binadamu wote ni Sawa, Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.Ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru." Kwa hiyo, vyama vina imani zake mbalimbali.

Je ni maendeleo gani ya kiimani tuyatakayo? Kama Waislamu, maendeleo ya kiimani tuyakayo ni kuwa na taifa linaloamini uwepo wa Mwenyezi Mungu Mmoja na sifa zake tukufu na kadhalika. Hivyo kwa kuzingatia imani hii, wale wanaodai kutaka kutuleteya maendeleo hawatopuuza mchango wa wale ambao wanatukumbusha uwepo wa Mwenyezi Mungu na muongozo wake kama ambayo hali ilivyo sasa hivi. Kwa mfano, kwa nini hamna walimu walioajiriwa kufundisha somo la dini mashuleni kama ilivyo masomo mengine? Je kwa nini serikali haitowi msaada katika kuchapa na kusambaza vitabu vya elimu ya dini mashuleni? Majibu mepesi tunayoweza kuyapata ni kuwa serikali haijihusishi na mambo ya dini au serikali haina dini. Ikiwa kuyafanya haya ni kujihusisha na mambo ya dini kana kwamba dini ni jambo baya kabisa basi ni wazi kuwa eneo hili la kimaendeleo limewachwa makusudi. Sisi tunaona kuwa serikali kama ambavyo inasimamia taasisi zote za dini bili kuziingiliya uendeshaji wake hivyo hivyo inayo nafasi ya kutowa machango wake katika eneo hili muhimu na nyeti la kimaendeleo. Hivyo, iwapo wanasiasa wetu wanadai na kuamini Mungu yupo, hatuna budi kuendeleza imani hiyo kwa kiwango cha kuthamini walimu wa masomo ya dini katika nchi yetu.

Maendeleo ya Kitabia

Mwanadamu anatabia zake za kimaumbile na zile anazojifunza kila siku na kuamuwa za kuchukuwa na kuziacha. Maendeleo yenye kubadilisha tabiya mbovu kuelekeya katika tabia nzuri (moral development) ni kipaumbele kinachostahiki . Je kama taifa tunafunza, kusimamiya na kuhimiza tabiya gani kwa wananchi wetu bila kujali mwanachama wa chama au la? Nchi yetu imeshuhudiya na inaendeleya kushuhudiya mmomonyoko wa maadili mema kwa vijana na wazee wetu. Haya ni matokeo ya kutofunza na kusimamia maadili ipasavyo katika ngazo zote. Watu wafunzwe tabia ya ukweli, uaminifu, uchapakazi, kufanya mambo kwa ajili Mungu n.k. Kama taifa tumewaachia watu fulani kufunza maadili kama vile viongozi wa dini, wazazi au mtu binafsi. Je inatosha? Jawabu ni haitoshi. Kama ambavyo tunafunza masomo ya uraia (civic education), mazoezi (physical education) n.k tunahitaji uwekezaji katika kufunza maadili mema kama taifa na kuyasimamia. Haitoshi kuwa na watu ambao wanasema "Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko" na kisha wanapoenda kinyume chake kwa kusema uongo hadharani na kuleta fitina ikawa taifa halichukuwi hatuwa zozote. Wamesema wanchuoni wa tabia kuwa "Taifa / Umma wowote ule kuwepo kwake na kubaki kwake kunategemeya uwepo wa maadili yake. Iwapo maadili yake yataondoka, basi na umma huo utakuwa umeondoka hata kama vizazi vingalipo."

Hivyo maendeleo tuyatakayo yawe jumuishi kwa watu wote, yenye mtazamo mpana na mtambuka ambayo yatajikita kumbadilisha mwanadamu mwenyewe kuwa kiumbe bora kama Mungu anavyotaka awe na kuimarisha mazingira yake na kustawisha jamii yote kwa ujumla. Maendeleo ambayo yanatowa fursa kwa wote kujiendeleza kwa uhuru bila uonevu wala kupendelewa au kukandamizwa. Maendeleo ambayo utu wetu unaheshimiwa, unalindwa, unaimarishwa na kuendelezwa na sio kudunishwa, kupuuzwa au kudumazwa.


Monday, July 20, 2020

HATARI YA MOTO NA HAJA YA BIMA YA KIISLAMU (TAKAFUL)



Mwaka wa 2019 na mwanzoni mwa mwaka huu, nchini Australia walipatwa na janga kubwa la moto katika misitu (bushfires) na mpaka katika makazi ya watu. Zaidi ya ekari 46 milioni ziliteketeya kwa moto, nyumba zaidi ya 3500 ziliunguwa na watu 34 walipoteza maisha.

Kwa masikitiko makubwa, mwezi huu baadhi ya shule za Kiislam kama vile Ilala Islamic, Mtambani, Kinondoni na kituo cha mayatima zilikumbwa na maafa ya kuunguwa kwa moto. Kwanza niwape pole wafiwa wa janga hili na waathirika wote wa moto huu na mingine iliyopita. Ni jambo la kusikitisha uhai na mali inapopoteya kwa mkasa wa moto au kwa janga lolote jingine. Kwa kuwa yameshatokeya, hatuna budi kuwa na subira na tunamuomba Mola atuepushe yasiendelee kutokeya maafa haya.

Binafsi nimekumbana na mtihani wa moto mara mbili katika maisha yangu. Mara ya kwanza, nikiwa shule ya msingi, nyumba yetu ilipatwa na mkasa wa kuunguwa na sehemu ya chumba kimoja iliathirika sana kisha moto huo ulizimwa kwa taufiki ya Allah kupitiya msaada ya majirani wema. Nakumbuka zahma na taharuki zake siku hiyo hazikuwa za kawaida. Mara ya pili, nikiwa chuo kikuu cha Kiislamu nchini Uganda, bweni letu lote lilichomeka kwa moto. Sikuweza kuokoa chochote zaidi ya nguo nilizokuwa nazo siku hiyo na ilikuwa karibu na muda wa mitihani ya kumaliza muhula. Ni mtihani mzito, uliotulazimu tulale msikitini kwa muda, tuazimwe nguo za kuvaa, kupewa nasaha (counselling) na mengi ya kueleza lakini hapa sio sehemu yake. Makala haya yatajaribu kusisitiza juu ya hatari ya janga la moto katika maisha yetu, athari yake kiuchumi na hatuwa za kuchukuwa ili kujihadhari na athari hizo.

Hatari na maafa ya Moto.

Maafa ya moto huenda yameanzia pale moto uliposhushwa na kutumika na binadamu ulimwenguni. Moto umetajwa katika vitabu vitukufu kama adhabu waliondaliwa waovu katika maisha ya Akhera kwa kuasi kwao maelekezo ya Mola wao. Ikiwa moto ni adhabu akhera kwa waovu, basi hili ni afa na janga kubwa na baya mno linaloweza kumpata binadamu duniani au akhera.

Siku moja wakati wa Mtume Muhammad s.a.w nyumba iliunguwa na kuunguza wakazi wake katika mji wa Madina. Mtume s.a.w akasema " Moto huu kwa hakika ni adui yenu. Mnapoenda kulala, hakikisheni mnazima sehemu zenye moto." (Sahih Bukhari). Katika hadithi nyingine kasema " Msiuwache moto unawaka katika nyumba zenu." Katika Qur'an, Allah s.w.t ametuagiza " Enyi Mlioamini, jiepusheni nyinyi na familia zenu kutokana na Moto." (66:6).

Vyanzo vya maafa ya kuunguliwa na moto ni anuai. Inaweza sababu ikawa ni hitilafu ya umeme (electrical), matumizi yasiyo sahihi ya majiko ya kuni, mkaa au gas (Cooking), sigara ambayo haikuzimwa, mishumaa na vifaa vya kutiya joto hasa katika maeneo ye baridi (heaters)na kadhalika. Kadhalika moto unaweza kusababishwa na watu wanaotaka kuhujumu wengine. Kimsingi, moto unapoleta maafa ni lazima vyombo vya uzimaji moto vifanye uchunguzi wa kina juu ya sababu yake na iwafahamishe wahusika sababu hizo. Katika nchi zilizoendeleya, matukio yote ya moto hurekeodiwa na sababu zake ili taarifa hizo ziwafae wananachi katika kuchukuwa tahadhari zaidi.

Athari za Kiuchumi.

Kuna nchi chache ambazo huweka taarifa ya gharama ya moto katika nchi zao kiuchumi. Nchini Uingereza na Wales, taarifa yao ya mwaka 2003 (Economic cost of fire report) imekisia kuwa gharama ya moto katika nchi hizo ni paundi 7.7 bilioni (sawa na Tzs 22 trilioni).

Katika moto uliotokeya Australia mwanzoni mwa mwaka huu, Wataalamu wa masuala ya bima walikisiya kuwa baina ya Nov 2019 mpaka kati ya Feb, 2020 moto huo ulisababaisha hasara inayokaribiya bilioni za marekani 1.3 kutokana na madai yaliyowasilishwa(insured claims) kwa makampuni ya bima. Mwaka 2015 katika nchi ya Indonesia, moto katika misitu yake na mazao yake yaliigharimu nchi hiyo dola za marekani bilioni 16.

Kiwanda kinapopata moto, wafanyakazi wenye ujuzi wanaweza kupoteza maisha yao, mashine na zama muhimu kuharibika, ajira kupoteya, uzalishaji kupunguwa n.k ni athari kubwa japokuwa sio rahisi kutathmini athari yake kifedha katika uchumi. Nyumba ya mtu inapatwa na janga hili, niwazi kuwa inamuathiri mtu kiuchumi kwa kukosa makazi yake salama na uwezekano wa kutumiya nyumba yake kama dhamana ya mikopo benki. Mbaya zaidi inamweka katika gharama ya kukodisha nyumba kila mwezi na kulipiya pesa kadhaa. Mifano hii michache itutosheleze kutambuwa kuwa moto iwe wa nyumbani au shuleni au kiwandani au ofisini unaathari kubwa kwa watu na mali zao na uchumi kwa ujumla.

Tathmini za awali za shule ya Ilala Islamic, Mvumoni na Kinondoni Muslim zinaonesha karibu nusu bilioni au zaidi zitahitajika ili kurekebisha hasara iliyojitokeza ya mali zilizopoteya lakini uhai hauwezi kurudi tena. Ikiwa taasisi hizo zinamkopo benki, wanaweza kuathirika katika kulipa mikopo na kusababaisha benki kuwa na mikopo mibaya (non-performing loans)


Hatuwa za kuchukuwa.

Kimsingi kuna hatuwa tatu za kukabiliana na tishio la moto katika nyumba au ofisi au kiwandani. Ya kwanza, ni kuchukuwa tahadhari ya kuepuka kuwa na matumizi ya moto kabisa katika nyumba au ofisi. Kusiwe na umeme, kusiwashwe kandili au mshumaa au matumizi ya kitu chochote cha moto, hii inaitwa ni ni kuepuka vyanzo vya hatari ya moto kabisa (risk avoidance). Hii ni njia ngumu kabisa kutekelezeka katika

Njia ya pili, ni kuendeleya na matumizi ya vitu vya moto na huku kuweka mitambo mbalimbali ya kugunduwa moto ukiwaka (fire sensors and alarms), njia za kuzimia maji za uhakika (fire water pipes), kamati za kuangalia na kutathmini majanga (crisis au disasters committees) ambazo zinaweza kuchukuwa hatuwa ya haraka janga linapotokeya n.k. Njia hii inalenga kupunguza athari ya uharibifu wa moto (risk reduction measure). Bado moto unaweza kutokeya na kuleta athari kiuchumi.

Njia ya tatu, ni kuhamisha athari ya kiuchumi ya janga la moto kwa kukata bima (Insurance -risk transfer). Kwa kupitiya bima ya moto, linapotokeya janga la moto katika nyumba au kiwandani au ofisini, kampuni ya bima itakuja kulipa gharama ya hasara iliyotokana na moto huo. Hivyo, bima inapunguza au kuondosha mzigo wa gharama ambazo zingehitajika kurekebisha nyumba au ofisi au kiwanda ili mwenyewe asikose makazi au asipatwe na gharama za kuijenga ofisi au nyumba kutoka mfukoni mwake. Lakini maisha ya watu hayawezi kurejeshwa kwa bima yoyote ile.

Kwa bahati mbaya na masikitiko makubwa, bima ya moto na zote zilizopo nchini ni HARAMU kwa waislamu kwa kuwa zinakwenda kinyume na sheria za mikataba ya biashara ya Kiislamu. Mikataba wa bima zilizopo unahusisha riba na kukosa uadilifu baina ya pande mbili. Jambo hili linawakera mno waislam na hasa ukizingatiya kuwa ipo njia mbadala nayo ni bima ya Kiislam (Takaful).

Harakati za kuomba kuwepo bima hii nchini zimeanza kitambo. Tangu mwaka wa 2012, mamlaka ya Bima (TIRA) ilifanya utafiti juu ya uwepo wa haja ya bima hii na utafiti huo ulionesha kuwa bima ya Kiislamu inahitajika nchini. Miaka iliyofuata mamlaka iliandaa taratibu za kutoa leseni na usimamizi wa bima aina hii (Takaful regulations) ambazo zilijadiliwa kwa kina na wadau na wataaalamu mbalimbali nchini hadi kuhitimishwa kwa ajili ya kusainiwa na kupelekwa Wizara ya Fedha. Mwaka 2018, katika mkutano wa kila mwaka wa Bima nchini uliofanyika Tanga, Waziri wa Fedha Mh. Mpango alikiri kuwa taratibu za bima hii zimechukuwa muda mrefu kukamilika na kuwa Waziri ataingilia kati (ministerial interventions) ili ziweze kusainiwa na kutumika.

Mwaka na miezi sasa tangu kauli hiyo itolewe, hatuna taratibu hizo na ilhali zipo kampuni ambazo zipo tayari jana kabla ya leo kuwekeza katika uendeshaji na utoaji wa bima hii nchini. Fursa za ajira zinapoteya na Mali za waislamu zinakosa bima ya Kiislamu mpaka kuangamiya kwa moto bila fidia kutokana na Waziri kushindwa au kulegalega katika kuidhinishwa kwa taratibu za bima hii. Hatutaki kuamini kuwa Waziri anashawishiwa na makampuni shindani yanayoona yatakosa biashara iwapo bima hii itaruhusiwa. Pia hatutaki kuamini kuwa Waziri hatambui haja na hamu kubwa ya Waislam na wananchi wote kuwa na bima yenye kusimama katika uadilifu.

Hivyo, tunamkumbusha kwa unyenyekevu mkubwa Waziri na wafanya maamuzi katika Wizara ya fedha, kuharakisha kupitishwa kwa taratibu hizo ili tuweze kupata wawekezaji zaidi katika huduma za bima nchini, kutengeza ajira, kuongeza matumizi ya bima kwa wananchi, kueleta ushindani na muhimu zaidi kuwawezesha waislamu kutumiya bima ambayo itawaezesha kupata fidia ya hasara za maafa ya moto na mengineyo.



Tuesday, July 14, 2020

UCHUMI WA KATI NA JAMBO LILILO MUHIMU ZAIDI


Siku chache zilizopita nchi yetu ilitangazwa kuwa sasa ni nchi yenye uchumi wa kati (middle income country). Wanasiasa wanaongoza serikali walitumiya fursa hiyo kudhihirisha furaha yao kwa kuona juhudi za muda mrefu zimezaa matunda. Wachumi wanaona hatuwa hii inafaida zake na hasara au changamoto zake. Na hili ni jambo la kawaida, iwe furaha kwa wanasiasa au iwe uchambuzi wa pande mbili -faida na hasara- kwa upande wa wachumi

Makala haya hayalengi kuwa upande wa wanasiasa wala wachumi wenye kupima maendeleo katika mizani ya pato la taifa. Makala haya inataka kubainisha kuwa pamoja na lengo hili la kuwa uchumi wa kati kufikiwa, tusisahau yaliyo muhimu zaidi na ambayo wenzetu waliondeleya (developed countries) wanalenga kulifikiya badala ya kuongezeka pato la taifa tu. Hii haimaanishi kuwa ongezeko la pato la taifa sio muhimu, la hasha. Lakini tufahamu kuwa ustawi wa nchi na watu wake haupo katika kuongeza kipato peke yake. Iwe kipato halisi au kama washindani waliokuwa nje ya serikali wanavyoona kuwa ni kipato cha katika makaratasi!

Wachumi wa Kiislamu kwa miaka mingi wamefikiria na kulenga katika kuelekeza sera za nchi katika kukuza kipato cha mwananchi kwa upande mmoja na kuhakikisha kuwa wananchi wanafuraha (Happiness). Hili la kipato linalenga kuhakikisha wananchi wanaondoka katika mtihani wa ufukara jambo ambalo
Mtume s.a.w alikuwa akimuomba Mola wetu amuepushe na ufukara. Na suala la kuwafanya watu wawe na furaha ni katika mafunzo ya Mtume s.a.w pale aliposema; amali au kitendo kizuri ni kufanya jambo kwa ndugu yako akafurahi au kuingiza furaha kwa ndugu yako!

Katika miaka ya 2010, wanasiasa na wachumi wa nchi zilizoendeleya wamezinduka kuona kuwa kile ambacho kwa miaka mingi wamekishughulikiya nacho ni kuongeza kipato cha watu wao,kuwa matajiri zaidi wakitarajiya kuwa kwa utajiri huo matatizo yote yatakwisha lakini la kustaajabisha ni kuwa pamoja na kuongezeka kipato katika nchi ya Amerika na Ulaya, lakini tafiti zinaonesha furaha haikuongezeka! Profesa Richard Layard na wenzake katika kitabu chao "The Origins of Happiness (2019)", wanauliza swali hili "jambo gani muhimu zaidi kwa mwanandamu (what matters most?) na kujenga hoja kadhaa kuwa fedha zilionekana kuwa ni muhimu mpaka hivi karibuni watu wakiipa fedha nafasi ya heshima. Lakini sasa hivi watu wengi duniani wameona na wanataka kutazamwa upya dhana ya maendeleo. Watu hawa wanakataa kuwa utajiri na kipato kuwa sera za maendeleo ya nchi na mtu binafsi yasiweke mbele zaidi kipato kikubwa kama ishara ya maendeleo na badala yake maendeleo yapimwe kwa kutazama watu wangapi wana furaha na maisha yao. Hivyo watunga sera wanapaswa kuzielekeza sera zao katika kuweka mazingira ambayo watu watakuwa na ustawi na furaha.

Kwa kulitambuwa jambo hili na umuhimu wake, nchi ambazo ni sehemu ya OECD wameazimiya kuwa sera za nchi zao zijielekeze katika ustawi na watu wao wawe na furaha. Hivi sasa kuna nchi kadhaa ambazo zimefikiya kuwa na mawaziri wa kuhakikisha watu wanaishi kwa furaha (Ministers for Happiness) kama vile UAE na sehemu nyingine. Umoja wa Mataifa umeifanya Machi 20 kila mwaka ni siku ya kimataifa ya furaha (International Day of Happiness).

Kadhalika tafiti na ripoti zimekuwa zikifanywa na kuchapwa kila mwaka ili kupima kiwango cha furaha cha wananchi wa nchi mbalimbali duniani. Kwa mfano ripoti ya mwanzo ilichapwa mwaka 2012 na ripoti ya mwaka huu -World Happiness Report 2020, inaonesha kuwa Tanzania ipo chini katika kuwa na watu wenye furaha! Bila shaka, ripoti hizo zinaweza kubishaniwa na hoja kutolewa za kuunga mkono au kuzipinga ripoti hizo. Ikiwa tutaziunga mkono au kinyume chake, jambo moja tunapaswa kukubaliana kama watanzania katika kuendeleza uchumi wa watu wetu nalo ni tusisahau yale ambayo yanawapa ustawi na furaha wananchi wetu! Jambo hili hatuna budi kulitazama kwa kina na kulipima wenyewe kila mwaka au baada ya miaka ili tuhakikishe kuwa kukuwa kwa kipato kunaenda sambamba na kuongezeka furaha na sio karaha au kuongezeka matatizo ya akili au watu kujitowa uhai bila sababu kama ilivyo leo katika nchi nyingi zilizoendeleya.

Katika kufikiya azma hii, Mtume s.a.w anatukumbusha na kutufunza aliposema "Katika mambo yenye kumpatiya mtu furaha ni kuwa na jirani mwema, kuwa na chombo kizuri cha usafiri na kuwa na makazi yenye nafasi."Wale ambao wamejaaliwa mambo hayo matatu basi wakithirishe kushukuru, na wale ambao wamekosa hayo, ni wajibu wa watunga sera kuweka mazingira mazuri ili vitu hivi avipate kila mwananchi wa Tanzania pamoja na kuwa na elimu bora na huduma bora za afya, maji safi, umeme wa uhakika, haki za binadamu zenye kuheshimiwa n.k. Tuanzie katika familiya zetu, mitaani, kata, vitongoji, vijijini, wilayani, mkoani na taifa lote kwa ujumla. Sote twenye dhima ya uongozi katika maeneo hayo, tutekeleze wajibu wetu wa kuweka mazingira mazuri ya ustawi na furaha!

Tuesday, July 7, 2020

UCHUMI WA KIISLAM NA UCHUMI WA KIBEPARI


Ulimwengu umeshuhudia aina kuu mbili za mifumo ya uchumi. Mifumo ya uchumi ya wanadamu na mfumo wa uchumi wa Mwenyezi Mungu. Watu walipojieka mbali na muongozo wa dini zao, waliunda dini mpya na mifumo mipya ya kuendesha maisha yao kwa kutarajiya kupata maendeleo au furaha au ustawi wa jamii zao. Je wameyapata maendeleo, furaha na ustawi wa jamii zao? Na je maendeleo au furaha au ustawi huo unaishia maisha ya dunia pekee au na maisha baada ya kifo? Yoyote yule anayejishughulisha na uchumi binafsi, wa jamii au wa nchi, yampasa ajiulize iwapo njia au mikakati anayofuata itampa utulivu duniani na malipo akhera. Hili ni suali muhimu ambalo yataka turudi katika kulinganisha baina ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na mfumo ya wanadamu kwa mfano ubepari (capitalism).

1. Itikadi.

Mfumo wa uchumi wa Kiislamu umejengwa na kusimama katika kuamini uwepo wa Muumba wa ulimwengu na walimwengu, Mwenye kuruzuku neema mbalimbali ni Mola mmoja asiyekuwa na mshirika. Ameumba ulimwengu kwa ajili ya matumizi ya mwanadamu na shughuli zake za kiuchumi hazina budi kutambuwa mchango wa Mola katika natija anayoipata. Je umeona moto ambao mnautumia? Je ni nyinyi ambao mlioanzisha au ni yeye? Je mmeona maji mnayokunywa? Ni nyinyi mlioyateremsha katika hazina zake au ni yeye? Je mmeona mbegu mnazozipanda ardhini? Je ni nyinyi mnaootesha mazao mbalimbali kwa mbegu hizo au ni yeye? (Surat Waqiah). Kiitikadi, mfumo huu unatambuwa kuwa yupo ambaye bila yeye hamna linalowezekana kwa juhudi ya mwanadamu peke yake. Hii haimaanishi kuwa mtu asijishughulishe, hapana afanye harakati mbalimbali za kujileteya maendeleo huku akijuwa kuwa hizo ni sababu tu na yeye Mola ndio anayesababisha sababu hizo zilete matokeo fulani. Hivyo, kwa kwa itikadi hii, yeyote anayejishughulisha katika kukuza uchumi wake na wa watu wake, hana budi vilevile kutambuwa mipaka iliyowekwa na yule ambaye ulimwengu ni milki yake. Kuna shughuli ambazo amezihalalisha na nyingine ameziharamisha. Hivyo uchumi wa Kiislam, unaona rasilimali zilizopo ni fadhila za Mola kwa wanadamu, zinatakiwa kutumika kwa njia ya halali, kuimarisha ustawi wa mtu na jamii yake na matokeo ya matumizi hayo daima yaambatane na shukrani kwa Muumba.

Mifumo ya uchumi wa kibinadamu inasimama katika kuamini kuwa ulimwengu umejitokeza tu bila kuumbwa na Mola. Nadharia mbalimbali za kuibuka kwa ulimwengu zimearifu kuwa Ulimwengu ulitokeya tu. Rasilimali hizi ni chache na hivyo hamna budi kufanya juhudi ya kila namna ili kuweza kuzimiliki rasilimali hizo kwa maslahi binafsi(ubepari) au maslahi ya jamii yote (ujamaa). Mfumo wa kibepari umeyaweka maendeleo na furaha na ustawi katika matashi na juhudi za mtu mwenyewe. Ni wewe mwenyewe unayeweza kujiendeleza au kujididimiza. Ukitumia rasilimali vizuri utapata natija nzuri au ukitumia rasilimali vibaya utapata matokeo mabaya, suala la uzuri na ubaya ni kwa mizani ya mwanadamu mwenyewe. Apataye ni mwerevu na aliyekosa ni mlegevu! Hamna la halali au haramu isipokuwa lile ambalo sheria za nchi imebainisha kuwa ni halali au haramu hata kama sheria hiyo inaenda kinyume na Sheria ya Mwenyezi Mungu. Hivyo, rasilimali zilizopo ni chache, ni zawadi ya asili, anayezimiliki ni mwerevu na kuzitumia rasilimali hizo ni kwa matashi binafsi ya kujipatiya furaha na ustawi kwa mtu binafsi bila kujali ustawi wa jamii nzima.

2. Uzalishaji Mali.

Mfumo wa uchumi wa Kiislamu unahimiza katika kuzalisha mali. Mali hiyo ni kila kitu chenye manufaa kwa watu katika maisha yao. Mali hiyo iwe ni zao la kazi ya halali na sio wizi au kwa hila mbalimbali. Mali inazalishwa kwa kulima, kuvua, kuzalisha, kutengeneza, kununuwa na kuuza n.k. Binadamu katika kuzalisha mali hana budi kuchunga asizalishe mali kwa njia za haramu au asizalishe mali haramu.

Mfumo wa kibepari pia unahimiza kuzalisha mali mbalimbali ili kupata utajiri ambao utatumiwa kwa maslahi ya mwenye mali mwenyewe. Mali hiyo ni kitu chochote kinachoweza kumilikiwa. Uzalishaji ni jambo huru kwa mtu kuamuwa mwenyewe anataka kuzalisha nini. Haidhuru kitu hicho kiwe ni kwa manufaa au chenye madhara kwa watu kwa mfano wa sigara, dawa za kulevya, ulevi, mirungi, filamu za ufuska, biashara ya bidhaa feki nakadhalika. Uhuru wa mtu ni kitu kitakatifu katika ubepari kiasi ambacho dola inawajibu wa kuulinda uhuru huo hata kama unamleteya madhara huyo mwenye kupewa uhuru huo. Hivi karibuni, huko amerika imekuwa halali kulima na kuvuta bangi katika baadhi ya majimbo ya nchi hiyo. Baada ya uzalishaji sigara, pombe na picha za ufuska, sasa bangi pia ni rukhsa na pengine wakaruhusu dawa za kulevya siku za usoni.

3. Matumizi ya Mali.

Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu unahimiza matumizi ya wastani ya mali na matumizi yenye kujali wengine. Mali uliyonayo ni amana kwa matumizi yako ya msingi na pia kuwatazama wengine. Uislam unakataza matumizi ya anasa na israfu na uharibifu wa mali. Kama ilivyokuwa katika kuchuma kwa kufuata amri za Mungu, na katika kuitumia pia ni lazima kufuta maelekezo ya Mungu. Mungu ameelekeza kuwa mali itumiwe kwa wastani kwa ustawi wa mwenye mali na familia yake, na jirani zake na jamii yake.

Mfumo wa kibepari unaona suala la matumizi ni eneo la uhuru wa mtu lisilokuwa na mipaka. Kama alivyotafuta kwa nguvu zake na matumizi ni kwa matashi yake. Hamna kizuizi katika matumizi isipokuwa sheria za nchi ambazo hata hivyo baadhi yake zinaonekana kuwa ni kandamizi dhidi ya uhuru wa binadamu. Mfumo huu kwa uhalisia unahimiza matumizi ya anasa na israfu na kununuwa vitu mara kwa mara (consumerism) kama njia ya kuthibitishia wengine kuwa wewe ni mwenye uwezo wa kumudu chochote ukitakacho. Mfumo huu unahimiza mashindano ya vitu badala ya utu. Wajibu wa mtumiaji mali unaishia katika kujistawisha na kujifurahisha yeye mwenyewe hata kama umezungukwa na majirani wanaolala na njaa au wanauguwa maradhi mbalimbali kwa kushindwa kumudu gharama za matibabau au kuishi katika ujinga kwa kushindwa kumudu gharama za elimu.

4. Usambazaji wa Mali.

Mfumo wa uchumi wa Kiislamu umeweka njia mbalimbali za kuigawa mali miongoni mwa wanajamii ili wote wawe na ustawi unaohifadhi heshima ya binadamu kama kiumbe bora ulimwenguni. Njia ya Zakat ni moja wapo. Kila mwenye mali analazimika kila mwaka kugawa sehemu ndogo ya mali yake kwa ajili ya wale ambao hawana kitu ili na wao waweze kufurahi na kustawi katika jamii yao. Mali inapaswa kuzunguka na sio kuhodhiwa na wachache! Njia nyingine ni sadaka na waqfu ambazo zinapelekeya mali kugawiwa kwa watu mbalimbai katika jamii ili kuinuwa hali zao.Serikali yenye kufuata mfumo huu, inajali raia wake kwa kuhakikisha wale ambao hawana uwezo wa kujikimu wanasaidiwa na serikali kupata mahitaji ya msingi yenye kuhifadhi utu wao na heshima yao.

Imesemwa kuwa Ubepari hauna roho. Kila kinachopatikana baada ya kutowa kodi stahiki (na mara nyingi kodi hiyo huepukwa kwa udanganyifu), mwenye mali hana wajibu wa kumsaidiya yoyote. Yoyote mwenye shida arudi kwa serikali yake, kwa msaada. Sio wajibu wa mfanyabiashara au mwenye mali kuhakikisha mali hiyo inawasaidia wengine katika jamii yake na hata kwa familia yake. Mzazi katika mfumo wa kibepari hana wajibu hata wa kumsaidia mwanawe aliyebaleghe kwa kumpa mtaji wa bure, mtoto katika umri huo ni wa serikali kumtazama na kujitafutia mwenyewe. Ni mimi mimi! (Man eat man society). Hakuna cha bure katika ubepari. Imesemwa ukipewa cha bure ujuwe wewe ndio bidhaa yenyewe ambayo inauzwa kwa wengine! Tunayaona haya katika mitandao ya kijamii. Ni bure kujiunga lakini kumbe taarifa zetu za kimtandao zinauzwa kwa pesa nyingi kwa wengine!


5. Fedha (Capital).

Mfumo wa uchumi wa Kiislam unaona kuwa fedha au mtaji unanafasi yake lakini sio mama wala msingi mkuu wa uzalishaji. Bali binadamu, mwenye nguvu kazi na maarifa akisuhubiana na mtaji unaohitajika hupelekeya katika uzalishaji na hivyo viwili hivyo havitengani katika uzalishaji. Fedha inahitajika kujumuika na binadamu mwenye maarifa na ujuzi katika uzalishaji wenye tija. Hivyo, vyote viwili vinatakiwa kuthaminiwa kwa uadilifu na bila kimoja kumuelemeya mwenzake kuwa ni eti ni bora zaidi. Hivyo ni marufuku katika uchumi wa Kiislam, mwenye fedha kutowa fedha kwa mkopo na kudai nyongeza bila kuwa tayari kubeba hasara inayotakana na shughuli inayofanyika na fedha hizo.

Ubepari (Capitalism) unaona kuwa fedha na mtaji ndio mama na msingi mkuu wa uzalishaji. Hivyo fedha pekee inaweza kuzalisha fedha nyingi zaidi kwa kokopeshwa kwa riba mara dufu na kumpatiya mwenye mtaji huo fedha zaidi bila kujali mchango wa binadamu katika kuzalisha. Watu ni watumishi wa mtaji na hivyo mtaji unastahiki kupata faida zaidi kuliko binadamu anayeufanya mtaji huo uzalishe zaidi. Kwa fikra hizi, ulimwengu leo unashuhudia mpasuko mkubwa sana baina ya matajiri na masikini. Kwa kuwa matajiri hao wanatumia mitaji yao katika kujipatiya faida kubwa kwa mfano wa riba hali ya kuwa wao wenyewe hawafanyi kazi yoyote. Mfumo huu hauzingatii uadilifu baina ya wenye mitaji na wenye kufanya kazi! Si ajabu Bilionea Ray Dalio, amesema kuwa "Capitalism is failing us (Ubepari unatufelisha katika maisha)."

Hitimisho.

Pamoja na kuwa uchumi wa Kiislamu ulishamiri katika wakati wa Mtume s.a.w na makhalifa zake waongofu na athari zake zikiwepo katika dola zilizokuwepo chini ya himaya ya Ukhalifa, leo ni nchi chache ambazo zina mwelekeo wa kushikamana na uchumi wa Kiislam. Habri nzuri ni kuwa mfumo wa uchumi wa Kiislam umekuwa ukifanyiwa utafiti kwa muda sasa ili uweze kufuatwa katika zama hizi baada ya kuwa ulipigwa vita baada ya kuanguka dola za Kiislam na kuingia ukoloni wa nchi za magharibi ambao ulifanya juhudi ili kufuta athari ya uchumi huu.

La kusukitisha zaidi ni kuwa binadamu katika zama hizi, wengi wetu tumekuwa mabepari na mifumo ya uchumi wetu imekuwa ikielekeya katika mfumo huo zaidi kuliko mifumo mingine. Hata hivyo, zipo tofauti katika mfumo huu wenyewe, kuna ubepari wa dola (State / political capitalism) ukiongozwa na China na ule wa nchi za kimagharibi (Liberal capitalism). Mwandishi wa Capitalism Alone, bwana Branko ameeeleza kwa undani kushamiri kwa aina hizi za ubepari na dosari zake akisisitiza kuwa mabadiliko lazima yafanyike haswa katika ubepari wa nchi za magharibi. Katika maependekezo yake, ameshauri dola zifanye yafuatayo:
1. Kuhamisha mitaji na umiliki wa mitaji hiyo kwa kuwapa nafuu ya kodi watu wenye vipato vya kati na kuwatoza kodi kubwa kabisa matajiri na kuweka kodi katika mali za mirathi. (deconcentrating capital and wealth ownership through tax advantages that give the middle class a bigger stake in financial capital and a corresponding increase in the taxation of the rich, coupled with higher taxes on inheritance).
2. Serikali zifanye uwekezaji mkubwa katika kuboresha elimu na kutowa fursa sawa kwa wazalishaji na wawekezaji. Hii inajumuisha serikali kufanya biashara na wawekezaji wa kati kwa kuwapatia tenda mbalimbali. (He also calls for a significant boost in public investment to broaden access to high-quality education and enhance equality of opportunity.)
3. Serikali kuweka kikomo cha michango ya matajiri kwa wanasiasa au vyama vyao na watunga sera mbalimbali ili matajiri hao wasihodhi mfumo wa kisiasa na kujinufaisha zaidi kupitiya wanasiasa ambao watakuwa wanawafungulia njia zaidi za kumiliki mitaji na kuwekeza pasi na ushindani ulio wa haki. (Strictly limited and exclusively public funding of political campaigns to reduce the ability of the rich to control the political process is another necessary reform).

Hizi ni hatuwa za mwanzo na mengi zaidi yanapaswa kufanywa ili kuiepusha nchi kama Tanzania, isije kujikwaa katika dosari za ubepari wa kimagharibi.


Sunday, June 28, 2020

BAJETI YA TANO NA MZIGO WA RIBA




Kama ilivyo kawaida, mwezi huu Mh. Waziri wa Fedha alisoma bajeti ya tano ya serikali. Bajeti hiyo imesifiwa na wadau mbalimbali kuwa ni bajeti nzuri na yenye ahueni kwa wananchi. Kwa hakika, uzuri wa kitu hujidhihirisha katika midomo ya watu na ahueni huhisiwa na watu. Pamoja na hayo, hakuna kazi binadamu ambayo yenye ukamilifu katika uzuri wake hata ikiwa tutataka na hakika hii inajidhihirisha katika maeneo mengi ya shughuli na kazi za binadamu.

Hivyo, bajeti ni nzuri lakini yapo maeneo ambayo kwa mtazamo wangu naona yatazamwe sana na kurekebishwa siku za mbele.

Eneo la kwanza, mzigo wa riba! Bajeti hii ni ya Trilioni 34.88. Katika matumizi ya bajeti hii, trilioni 22.10 au 63% ni za matumizi ya kawaida na asilimia 37% ni za matumizi ya maendeleo. Katika hii trilioni 22, trilioni 2.8 au 12% ni malipo ya riba peke yake, ukiongeza za mtaji utakaolipwa inafika trilioni 8.5 au asilimia 38% ya bajeti ya matumizi inaenda kulipa deni na riba zake.

Na mwaka huu serikali inatarajiya kukopa trilioni 4.9 kutoka katika soko la ndani. Hii itaongeza deni na itaongeza riba. Katika kiasi hicho, trilioni 3.32 sawa na 67% ya mkopo huu wa tril 4.9 ni kwa ajili ya kulipa madeni ya nyuma yalioyoiva (you borrow from John to pay Tom) na kiasi kilichobaki ni kwa ajili ya shughuli za maendeleo. Tukirudi katika nukta ya msingi ni kuwa tuna riba ya tril 2.8 ya kulipa mwaka huu peke yake. Tril 2.8 ni pesa nyingi kwa taifa letu kulipa kama Riba. Kwa mfano, bajeti yote ya elimu ni trilioni 1.3, Wizara ya Afya peke yake ni Bilion 933. Hivyo riba tunayolipa ingeweza kuongeza bajeti yetu ya elimu na Afya, na kubakiwa na chenji!

Nilifanya hesabu ndogo kuona kila mwananchi analipa riba ya kiasi gani. Hivyo tril 2.8 ukigawa kwa watu takribani milioni 57, ni kiasi cha riba ya Shilingi elf 49 ambayo kila mmoja wetu anachangia katika riba hiyo itakayolipwa. Hivyo, kila mmoja wetu anataka au la, japokuwa baadhi yetu ni dhambi kubwa sana kukopa na kulipa mikopo ya riba hata iwe ni kwa sh 10, tunalipa kiasi hicho kwa kupitia kodi zetu mbalimbali. Hivyo ni dhahiri, ubunifu unahitajika katika sera zetu za fedha katika suala la ukopaji na tukiongozwa na kumuogopa Mungu aliyeharamisha riba, basi tutapata njia.

Wenzetu wa Sudan na Irani, wameiepuka riba kabisa katika uendeshaji wa nchi zao. Hivyo,inawezekana! Naiomba serikali ijitahidi kubuni njia zisizo za riba kwa kujifunza kutoka katika nchi hizo na Malaysia n.k, ili kugharamia miradi ya maendeleo nchini. Rais Obasanjo amepata kusema "If you ask me what is the worst thing in the world, I will say it is compound interest.(Ukiniuliza mimi, kitu kibaya zaidi ulimwenguni, nitasema kuwa ni riba juu ya riba!)” Pope Francis amesema "“Usury humiliates and kills (Riba inadhalilisha na kuuwa).” Pia amesema, “Usury is a grave sin. It kills life, stomps on human dignity, promotes corruption, and sets up obstacles to the common good. (Riba ni dhambi kubwa, inaua maisha, inachafuwa heshima ya mwanadamu, inashawishi ufisadi na ni kizuizi cha kufanya mambo mema.” (https://www.vaticannews.va/en/pope/news/2018-02/pope-francis-usury-financial-exploitation.html).

Katika Uislam, riba ni dhambi yenye kuangamiza. Anayejihusisha na riba ametangaza vita na Mungu! Ni wazi vita hivyo sio rahisi mwanadamu kuishinda. Tuachane na njia hii ya kukopa kwa Riba kama serikali, kama biashara na kama wananchi!

Eneo la pili, ni katika suala la kuondosha kampuni za mawasiliano zinazomilikiwa na serikali kwa 25% na ziada katika takwa la kuorodheshwa katika soko la hisa. Pia kuziondoa kampuni zenye kumiliki minara ya mawasiliano zisiwe sehemu ya makampuni yanayotakiwa kuorodheshwa katika soko la hisa la Dar es salaam. Pendekezo hili waziri ameeleza mantiki yake ni kuhakikisha serikali inabaki na hisa hizo na kupata faida zaidi badala ya kuzipunguza iwapo kampuni hizo zitaorodheshwa katika soko la hisa. Tukifuata mantiki hii, hatutoweza kulikuza soko la hisa ipasavyo kwa kuwa inaonesha kuwa serikali ni mchoyo (state is greed) katika hisa zake katika makampuni ya mawasiliano na hivyo wenye makampuni ya binafsi hawatashawishika kuuza hisa za makampuni yao hapo. Kama serikali ni yenye uchoyo, watu binafsi ni wachoyo zaidi. Kampuni zinazofanya vizuri hazitaona haja ya kuwashirikisha watanzania katika umiliki wa makampuni yao.

Kwa upande mwingine kwa sasa makampuni yaliyopo katika soko la hisa ni machache (27 hivi) wakati Kenya wana zaidi ya makampuni 60. Tunahitaji kutengeza vishawishi (incentives) kwa makampuni mazuri wajiorodheshe katika soko letu hili. Na Mh. Waziri alisema katika bajeti hii kuwa serikali inalenga kutowa elimu ya umma ili kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika soko la hisa. Ili lengo hili litimie panahitajika kuwa na uwanja mpana wa makampuni ya kuwekeza. Hebu tafakari iwapo tu watu milion 20, watazikimbilia hisa za kampuni 27 wangapi watapata na wangapi watakosa? Kwa hivyo tunahitaji kuongeza makampuni katika soko la hisa na sio kuzizuia kisheria baadhi zisifanye hivyo. Sasa jambo hili la kuziondoa baadhi ya kampuni, linahitaji kufikiriwa vizuri zaidi na haswa kuweka mikakati yenye kushawishi kampuni nzuri binafsi za ndani na nje ya nchi zijiorodheshe katika soko la hisa.

Kwa leo ningependa kuishia hapa. Ni matumaini yangu kuwa nasaha hizi zinaweza kusaidia nchi yangu na watu wake.


Thursday, May 21, 2020

KUDHIBITI BEI (TAS'IR) KATIKA UISLAM


Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikiya juu ya serikali kuwataka wafanyabiashara wauze bidhaa fulani za chakula kwa bei elekezi. Vile vile kuna bidhaa ambazo tangu kuingizwa kwake sokoni bei huwa imeshapangwa na serikali kama vile mafuta ya petroli n.k. Bidhaa nyingine bei hupangwa na nguvu ya soko (market forces).

Mwanzoni wa mwezi huu tumesikiya juu ya kuadimika kwa sukari jambo ambalo serikali imelikanusha kuwa sukari ipo lakini kuna watu wemeihodhi kwa manufaa yao binafsi. Na upande mwingine kuna taarifa kuwa viwanda kadhaa vipo katika kurekebisha mitambo yao na pia kutokana na mvua kubwa zinazoendeleya nchini Tanzania kumepelekeya miwa kutokuwa na sukari ya kutosha. Ili kukabiliana na uhaba huo hatuwa zifuatazo zimechukuliwa:

1. Serikali imeagiza sukari kutoka nchi ya jirani ya Uganda.
2. Serikali kuwataka wafanya biashara wauze kwa bei elekezi ya serikali. Bei za sukari ni kama ifuatavyo, Iringa (2900), Mbeya (3,000), Rukwa, Katavi, Ruvuma (3,200), Njombe (2,900), Lindi, Mtwara (2,800), Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Tanga (2,700), Dar (2,600), Pwani, Morogoro (2,700), Kagera, Mwanza, Shinyanga,Simiyu, Geita (2,900), Mara (3,000), Kigoma (3,200), Singida, Tabora, Dodoma (2,900), Songwe (3,000). Wale waliokutwa wakiuza bei ya juu, hatuwa kadhaa zimechukuliwa ikiwemo:

a. Kufunga maduka ya wafanya biashara waliokiuka bei hiyo elekezi. Huko Kigoma, Mkuu wa Mkoa aliwafungia wafanya biashara watano kwa kuuza bei zaidi ya iliyoelekezwa.
b. Kupigwa faini au adhabu ya kupokonywa leseni na kupigwa faini.

Utetezi wa wafanyabiashara waliokamatwa ni kuwa sukari imeadimika na kuwalazimu kuinunuwa kwa bei ya juu ili kuweza kuisambaza bidhaa hiyo kwa wananchi na wao kupata faida kidogo (bei elekezi 3200 wao wanauza 3700 kwa Kigoma). Ikumbukwe kuwa tatizo hili sio mara ya kwanza kujitokeza. Mwaka 2014 jambo hili lilijitokeza tena na pia miaka ya nyuma.

Suala la kudhibiti bei ni nyeti, la kiuchumi na kidini. Uislam unasemaje kuhusu kudhibiti bei kupitiya vyombo vya dola / serikali? Uislam haujaliwacha suala hili bila muongozo wake. Kimsingi, bei hupatikana kwa njia mbili.

1. Nguvu ya Soko (market/ natural forces). Allah s.w.t ndie mwenye nguvu ya kufanya bidhaa fulani iwepo au isiwepo na pia ndie mwenye uwezo wa kufanya watu wahitaji bidhaa fulani au wasihitaji, kwa kuwa anadhibiti nyoyo za viumbe vyake na anafanya anavyokataka. Hivyo yeye Mola ndio anayedhibiti bei za bidhaa kwa kupitia uwezo wake wa kuruhusu bidhaa iwepo au isiwepo (supply side) na pia kudhibiti uhitaji wa bidhaa hiyo sokoni (demand side). Hivyo, pande mbili hizi zinapokutana na kuwafikiana bei wenyewe bila mtu yoyote wa tatu kuingilia.

2. Kupitia bei elekezi za serikali kwa ajili ya kulinda maslahi ya ummah. Hivyo serikali inaweza kutowa maelekezo ya bei kwa bidhaa au huduma fulani. Njia hii ya serikali kupanga bei ni suala lenye ikhtilafu wa wanazuoni. Wapo wanaowafiki kwa masharti na wanakaotaa kuwa serikali isiingilie bei ya soko.

Serikali huingilia bei ya soko ( intervene) kwa kutowa maelekezo ya bei ya bidhaa au huduma husika kwa lengo la kumlinda mnunuzi wa mwisho. Hamna ambaye anamashaka na nia njema ya serikali katika kupanga bei. Njia hii ndio inaitwa Taasir. Imam Shafii anaeleza kuwa Tas'ir ni hali ambayo serikali inatowa amri ya kuuza bidhaa kwa bei kadhaa katika soko.

Baadhi ya wanachuoni wanaona kuwa moja ya wajibu wa serikali ni kupanga bei ya bidhaa muhimu inapokuwa kuna haja ya kufanya hivyo. Na wapo wanaoona kuwa kimsingi, katika suala la kuendesha uchumi, wajibu wa serikali sio kupanga bei bali kuhakikisha hamna mwenye kuhodhi bidhaa au wenye kufanya ubabaishaji na kuhakikisha kuwa bei za sokoni zinaenda kwa mujibu wa nguvu ya soko bila ya kuwepo haja ya serikali kutowa bei elekezi. Kwa sababu Mtume s.a.w amesema kuwa "...bei hupangwa na Mungu, ndie mwenye kuzuia na kukunjuwa rizki kwa waja wake..." [Hadithi Sahih]

Hadithi hiyo huchukuliwa kama hoja dhidi ya serikali kupanga bei. Hata hivyo, wapo wanao ona kuwa muktadha wa hadithi hiyo ni kuwa katika hali ya kawaida hamna haja ya kuingilia na kuelekeza bei ya bidhaa sokoni. Lakini hadithi hii haizuii serikali kuingilia kati pale inapodhihiri kuwa kuna kuhodhi soko (monopoly) kwa wazalishaji au wauzaji wachache kwa manufaa binafsi. Ikibainika jambo hilo ndipo inadhihiri haja ya serikali kupanga bei kwa:

-----Kuunda mamlaka maalumu yenye wajuzi wa masuala ya bidhaa na masoko ili kusimamia bei za bidhaa husika sokoni. Wajuzi hawa watafanya tafiti zao kubaini chanzo cha bei kupanda au kushuka isivyokawaida na baada ya kubaini visababishi vyote vya hali hiyo wataweka bei ya sawa na haki inayozingatiya gharama (cost) na faida (profit). Bei hiyo iwe ni ya uadilifu na haki, pia iwafikiwe na wahusika-wazalishaji na wanunuzi. Katika kufanikisha hili pande zote zizingatie kuheshimiana, kuhurumiana na kuvumiliana.


Izingatiwe kuwa kuhodhi bidhaa ni kinyume na Sharia pale mtu anapohifadhi ghalani bidhaa inayohitajika ili kutengeza upungufu na kunyanyuwa bei ya soko kwa makusudi. Hata hivyo, mkulima hatakiwi kushurutishwa kuuza bidhaa zake sokoni. Kazalisha mwenyewe na hivyo anahaki auze au la. Vilevile watengezaji wa bidhaa za ubunifu, wana haki ya kuamuwa wauze au la na muda gani. Ni haki yao hiyo. Lakini wazalishaji wa viwandani (producers) au wafanyabiashara (traders) hawatakiwi kuzuia ghalani bidhaa zao kwa sababu ya kutaka kupata faida kubwa.

Fikra za wanazuoni kuhusu Taasir.

Kimsingi, kati hali ya kawaida ni haramu serikali kuweka bei elekezi za bidhaa na huduma bila ya kuwepo haja yoyote ya kufanya hivyo. Huu ni mtazamo wa maimam wanne, pia Ziaidiya na Imamiyah. Hii ni kwa sababu, suala la mauziano ni mawafikiano ya pande mbili kwa hiari yao. Haifai pande moja kushurutishwa kuuza au kununuwa kwa bei fulani.

Katika zama za Mtume iliwahi kutokeya watu kumfuata ili apange bei. Hali iliyokuwepo ni kuwa bidhaa iliadimika sokoni na mahitaji yaliongezeka. Hapakuwa na makubaliano ya kibinafsi ya wauzaji wala kuhodhi mali. Kwa hali ya kawaida ni kuwa, kunapokuwa na ongezeko la mahitaji na uchache wa bidhaa, bei hupanda. Mtume s.a.w alikataa kupanga bei ilipotokeya bei kwenda juu akisema "bei hupangwa na Mungu, ndie mwenye kuzuia na kukunjuwa riziki kwa waja wake. Mimi nataka nikutane na Mola wangu nikiwa sina haki ya mtu mwingine iwe katika damu yake au mali yake!"

Pamoja na msimamo huo, wanazuoni wametofautiana kuhusu wajibu wa serikali kupanga bei katika hali isiyokuwa ya kawaida (exceptional cases) ili kuhifadhi maslahi ya ummah. Kuna makundi matatu au rai tatu katika jambo hili:

1. Imam Abi Hanafa, anachukulia kuwa ni Makruh Tahrimi (jambo lisilopendeza linaloekeya katika katazo).
2. Imam Shafii, anachukuliya kuwa ni haramu kupanga bei iwe kuzipandisha au kuzishusha katika hali yoyote iwayo.
3. Imam Hanbali, wao wanatofautisha aina mbili za kupanga bei- kwa haki na kwa dhulma. Kupanga bei kwa haki kunaruhusiwa na kwa dhulma ni haramu.

Imam Shawkani, anaona kuwa tas'ir ni haramu kutokana na matumizi ya nguvu na ubabe unaotumika ndani yake. Hii ni kwa sababu kila mtu anahaki na mali yake na hivyo kupanga bei ni kuingiliya haki hiyo. Kadhalika Imam Ibn Hazm na Al Mawardi, wanapinga kabisa kupanga bei za bidhaa kwa hali yoyote ile na kwa bidhaa yoyote ile, iwe bei imepanda au imeshuka.

Hivyo, wale wanaokataa kupanga bei wanafuata maana ya hadithi iliyotajwa hapo juu na wale wanaoona kuwa kuna mazingira yafaa na wakati mwingine haifai, imetokana na Ijtihadi zao kwa kuzingatia hali ilivyo. Wao wanaona kuwa Mtume s.a.w hakupanga bei kwa sababu masoko yaliendeshwa kwa uadilifu. Wauzaji hawakufanya hila yoyote katika kupanda kwa bei na hivyo basi iwapo itaonekana kuwa kuna hila ya wauzaji basi mtawala anaweza kuingiliya kati ili kulinda maslahi mapana ya umma. Lakini ikiwa ni kutokana na kuadimika kwa bidhaa husika sokoni bila kufichwa na wauzaji au kuongezeka kwa hitajio la watumiaji ni haramu kupanga bei katika hali hiyo.

Hivyo kuna hoja tatu za wanaopinga kupanga bei.
1. Haifai kumlazimisha muuzaji kuuza kwa bei asiyokuwa radhi nayo. Mtume s.a.w amesema "Haifai kula mali ya Muislam ila kwa kuridhiya mwenyewe kwa nafsi yake.
2. Mtume s.a.w aliombwa apange bei na alikataa kufanya hivyo.
3. Ni dhulma kumlazimisha mtu mwenye mali yake kuuza kwa bei asiyoridhiya.
4. Inaweza kuchangiya kuibuka kwa soko la kificho (black market) kwa sababu ya kuminya uhuru wa wazalishaji au wauzaji kuuza kwa bei waitakayo.

Kwa upande wa wanachuoni wanaona kuwa inafaa kupanga bei, wameweka masharti katika kufanya hivyo. Ibn Taymiyyah anawafiki kupanga bei ya haki iwapo jambo hilo litapelekeya kusimamisha haki hasa pale iwapo watu hawatoweza kupata mahitaji yao ya msingi isipokuwa kwa njia ya kupanga bei ya haki (fair price) na inapokuwa imethibiti kuwa wafanya biashara wanafanya hila kwa ajili ya kujinufaisha. Hatahivyo, mpangilio uliowekwa na wanachuoni hawa ni kuwa ipatikane jopo la wataalamu watakaotazama chanzo cha mtikisiko wa bei na kuja na ufumbuzi kwa njia ya mashauriano na sio kwa njia ya kulazimisha na ubabe (by force and tyranny).

Hivyo basi iwapo fikra ya kupanga bei haina budi kufuatwa, mashauriano ya kina (public and private dialogue) katika kutafuta chanzo na suluhisho ni muhimu kabla ya watumishi wa serikali kufika katika maduka ya watu na kutowa adhabu na kuwaharibia heshima zao wafanyabiashara hao kwa kuwatuhumu na kuwaadhibu kwa wakati mmoja. Watumishi wa serikali wakiwa na mashaka na wafanyabiashara ambao wanahodhi, njia nzuri ni kuwapeleka mahkamani. Adhabu ibaki kuwa ni eneo la mahkama kuamuwa. Muuza duka mtaani kutofuata bei elekezi ya serikali haipendezi lakini je ni haki kufuata bei elekezi yenye kumpatia hasara au kumfungiya mlango wake wa riziki? Pia imedhihirika kuwa serikali inazo njia nyingine za kukabiliana na upungufu wa bidhaa iwe kutokana na kuhodhi kwa wafanya biashara au kwa kuwepo ongezeko la mahitaji, nayo ni njia ya kuagiza bidhaa hiyo kwa wingi kutoka nchi nyingine.

Kwa kuhitimisha, natarajiya kuwa watendaji wa serikali wamche Mungu zaidi wakijuwa kuwa suala la kupanga bei sio jepesi, kuingiliya mali ya mtu binafsi sio jambo jepesi. Muhimu zaidi ni kuwa njia yakuagiza kutoka nje, kuwadhibiti wanaohodhi na kuwa na jopo la wataalamu kwa ajili ya mashauriano inapaswa kuzingatiwa sio kwa bidhaa za mafuta pekee bali hata kwa mazao mbalimbali inaodhihiri haja ya kufanya hivyo.